Nazareti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kisima cha Bikira Maria - Kisima cha karne ya 1 ni kielelezo cha mji wa Nazareti.

Nazareti (الناصرة kwa Kiarabu, נצרת kwa Kiebrania) ni mji wenye watu 77,445[1] upande wa kaskazini wa nchi ya Israeli, ambao kihistoria unajulikana kama Galilaya.

Wakazi wengi ni raia wa Israeli wanaoongea Kiarabu na kufuata dini za Uislamu (68,7%) na Ukristo (31,3%).

Nazareti unajulikana kama mji walipokulia Bikira Maria na mwanae Yesu Kristo, ambaye kadiri ya Injili, ingawa alizaliwa Bethlehemu, alikuwa anatajwa kama Mnazareti.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Population in the Localities 2019" (XLS). Israel Central Bureau of Statistics. Retrieved 16 August 2020.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]