Bethsaida

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bethsaida

Bethsaida (kutoka Kiebrania/Kiaramu בית צידה beth-tsaida, yaani "Nyumba ya uwindaji" au "ya uvuvi", kutoka mzizi צדה auצוד)[1] ni mahali panapotajwa na Agano Jipya.

Palikuwa upande wa mashariki wa mto Yordani, labda jirani na mahali ambapo mto huo unaingia katika Ziwa Galilaya. [2]

Bethsaida ndio mji asili wa mitume wa Yesu wafuatao: Petro, Andrea nduguye na Filipo (Yoh 1:44).

Bethsaida inatajwa na Mk 8:22-26 kama mji (κώμη) ambapo Yesu alimponya kwa awamu mbili mwanamume kipofu.

Ingawa katika Injili hakuna habari za miujiza mingine iliyofanyika huko, Yesu aliutishia mji huo laana ya milele kwa kutopokea ujumbe wake wa toba.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.biblicaltraining.org/library/bethsaida-beth-saida
  2. (Ant., XVIII, ii, 1; BJ, II, ix, 1; III, x, 7; Vita, 72)

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Coordinates: 32°54′36″N 35°37′52″E / 32.910°N 35.631°E / 32.910; 35.631

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bethsaida kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.