Nenda kwa yaliyomo

Mtume Filipo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kifodini cha Mt. Filippo, 1639, José de Ribera.
Kaburi la Mtume Filipo huko Hierapoli.
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Filipo (kwa Kigiriki Φίλιππος, Philippos) ni jina la mfuasi wa Yesu Kristo anayeshika nafasi ya tano katika orodha zote nne za Mitume wa Yesu katika Agano Jipya.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu na Kanisa Katoliki na madhehebu mengine yote ya Ukristo yanayokubali heshima hiyo, lakini kwa tarehe tofauti. Kwa Wakatoliki ni tarehe 3 Mei pamoja na Yakobo Mdogo [1][2]

Habari zake zinapatikana hasa katika Injili na Matendo ya Mitume.

Mtu wa Bethsaida, kama Mtume Petro, alikuwa mfuasi wa Yohane Mbatizaji alipoitwa na Yesu amfuate [3]. Ndiye aliyemletea rafiki yake Natanaeli wa Kana (Injili ya Yohane 1:43-46).

Baadaye aliulizwa na Kristo bei ya mikate inayohitajiwa na umati kabla hajawazidishia ile michache iliyokuwepo (Yoh 6:5-7}.

Pia alimletea Yesu Wagiriki ambao walifika Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka wakataka kumfahamu (Yoh 12:20-22).

Hatimaye, katika karamu ya mwisho ya Yesu na mitume wake alimuomba awaonyeshe Baba (Yoh 14:8) akalaumiwa naye kwa kutomtambua ndani yake (Yoh. 14:9).

Eusebi wa Kaisarea, katika Historia ecclesiastica, iii.39, aliripoti maneno ya Papias, askofu wa Hierapoli kwamba Filipo alikuwa na mke na watoto na kwamba alifia dini Hierapoli (mwaka 80 hivi).

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/94044
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/20950
  • Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 154-155
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 131-132
  • Maurice Soseleje, Kalendari yetu – Maisha ya Watakatifu – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1986 – ISBN 9976-63-112-X, uk. 39

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtume Filipo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.