Yuda Iskarioti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Busu la Yuda kwa Yesu bustanini lilivyochorwa na Beato Angelico
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Yuda Iskarioti (kwa Kiebrania יהודה איש־קריות), Myahudi wa karne ya 1, alikuwa mmojawapo wa Mitume wa Yesu, maarufu kwa kuwa alimsaliti mwalimu wake apate vipande thelathini vya fedha (Injili ya Mathayo 26:14-16).

Ni tofauti na mtume mwenzake Yuda Tadei.

Majina[hariri | hariri chanzo]

Kwa Kigiriki, katika Agano Jipya anaitwa Ιουδας Ισκαριωθ (Ioudas Iskariôth) na Ισκαριωτης (Iskariôtês).

Kwa kuwa Yuda ni jina la babu wa kabila kubwa la Israeli lililobaki baada ya yale ya Kaskazini kupotea uhamishoni (722 KK), lilitumiwa sana na Wayahudi, hata wawili kati ya mitume hao wanaitwa hivyo.

Ndiyo sababu ilibidi kuwatofautisha kwa jina la pili, ambalo kwake ni "Iskarioti", maana yake "mtu wa Kariot" (Ish Kariot) kutokana na kijiji cha asili (Keriot-Chezron kinachotajwa tu katika Kitabu cha Yoshua 15:25, kikiwa Kusini kwa Yudea, mipakani kwa Edomu, kwenye Neghev.

Tafsiri nyingine inategemea jina Ekariot ("gaidi") walilopewa wapiganiauhuru wakali zaidi, waliokuwa tayari kuua wakoloni popote pale.

Tafsiri ya tatu inazingatia neno la Kiaramu sheqarya' au shiqrai, linalomaanisha mtu dhalimu; "tapeli" linaweza kutafsriwa ishqaraya.

Tafsiri ya mwisho inategemea neno lingine la lugha hiyo, sakar, yaani anayekabidhi.

Katika Agano Jipya[hariri | hariri chanzo]

Yuda anatajwa katika Injili na mwanzoni mwa Matendo ya Mitume.

Humo tunasoma kwamba alikuwa mwekahazina wa kundi la Mitume (Injili ya Yohane 12:6) mwenye tabia ya udokozi ambaye hatimaye alimuuza Yesu Kristo kwa maadui wake wa Baraza la Israeli (Injili ya Mathayo 26:47-49).

Mapema baada ya tukio hilo alikufa vibaya (30 B.K.) na nafasi yake ikashikwa na Mtume Mathia.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yuda Iskarioti kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.