Nenda kwa yaliyomo

Yuda Iskarioti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Busu la Yuda kwa Yesu bustanini lilivyochorwa na Beato Angelico
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Yuda Iskarioti (kwa Kiebrania יהודה איש־קריות), Myahudi wa karne ya 1, alikuwa mmojawapo wa Mitume wa Yesu, maarufu kwa kuwa alimsaliti mwalimu wake apate vipande thelathini vya fedha (Injili ya Mathayo 26:14-16).

Ni tofauti na mtume mwenzake Yuda Tadei.

Kwa Kigiriki, katika Agano Jipya anaitwa Ιουδας Ισκαριωθ (Ioudas Iskariôth) na Ισκαριωτης (Iskariôtês).

Kwa kuwa Yuda ni jina la babu wa kabila kubwa la Israeli lililobaki baada ya yale ya Kaskazini kupotea uhamishoni (722 KK), lilitumiwa sana na Wayahudi, hata wawili kati ya mitume hao wanaitwa hivyo.

Ndiyo sababu ilibidi kuwatofautisha kwa jina la pili, ambalo kwake ni "Iskarioti", maana yake "mtu wa Kariot" (Ish Kariot) kutokana na kijiji cha asili (Keriot-Chezron kinachotajwa tu katika Kitabu cha Yoshua 15:25, kikiwa Kusini kwa Yudea, mipakani kwa Edomu, kwenye Neghev.

Tafsiri nyingine inategemea jina Ekariot ("gaidi") walilopewa wapiganiauhuru wakali zaidi, waliokuwa tayari kuua wakoloni popote pale.

Tafsiri ya tatu inazingatia neno la Kiaramu sheqarya' au shiqrai, linalomaanisha mtu dhalimu; "tapeli" linaweza kutafsriwa ishqaraya.

Tafsiri ya mwisho inategemea neno lingine la lugha hiyo, sakar, yaani anayekabidhi.

Katika Agano Jipya

[hariri | hariri chanzo]

Yuda anatajwa katika Injili na mwanzoni mwa Matendo ya Mitume.

Humo tunasoma kwamba alikuwa mwekahazina wa kundi la Mitume (Injili ya Yohane 12:6) mwenye tabia ya udokozi ambaye hatimaye alimuuza Yesu Kristo kwa maadui wake wa Baraza la Israeli (Injili ya Mathayo 26:47-49).

Mapema baada ya tukio hilo alikufa vibaya (30 B.K.) na nafasi yake ikashikwa na Mtume Mathia.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yuda Iskarioti kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.