Nenda kwa yaliyomo

Mwanakondoo wa Mungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Agnus Dei ya Karne za kati katika Basilika la Parenzo, Korasia.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Mwanakondoo akishika bendera ya Kikristo ni ishara ya Yesu mshindi.

Mwanakondoo wa Mungu ni neno la Injili ya Yohane (1:29, 36) lililotamkwa na Yohane Mbatizaji kumhusu Yesu Kristo ili kumtambulisha kama kafara itakayotolewa kwa ukombozi wa binadamu wote: kwamba atabeba dhambi ya ulimwengu mzima na kuifidia kwa kujitoa kabisa.

Kwa Kilatini neno hilo ni Agnus Dei na linatumika kutajia mchoro wa mwanakondoo mwenye msalaba (au bendera ya msalaba) ukiwa ishara ya Kristo.

Agnus Dei ni pia jina la litania fupi ambayo inaanzia na maneno hayo na kutumika wakati wa Misa padri anapomega hostie takatifu na kuchanganya kipande na umbo la divai lililomo katika kikombe.

Litania fupi ya namna hiyo inapatikana pia katikati ya utenzi maarufu kwa jina la Kilatini "Gloria".

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mwanakondoo wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.