Waluo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Waluo (pia Wajaluo) ni kabila hasa la Kenya. Wako pia Uganda ya msahriki na wachache wanaishi nchini Tanzania katika Mkoa wa Mara. Lugha yao ni Kiluo. Wenyewe hujiita Jaluo na lugha yao Dhulou.

Waluo ni mkusanyiko wa kabila la kinilotiki ambalo lilisafiri kutoka Afrika ya Kaskazini kufuata mto Nile kuja Kusini. Waluo wengi wameenea kandokando ya Ziwa Viktoria kutokana na utamaduni wao wa uvuvi. Kwa Afrika mashariki utawakuta nchini Sudan, Kenya, Uganda na Tanzania.

[hariri] Waluo mashuhuri

WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Waluo" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Waluo kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.