Wakadam

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wakadam ni kabila la watu wanaoishi kwenye mlima Kadam, kaskazini-mashariki mwa Uganda (wilaya ya Nakapiripirit). Walikimbilia huko baada ya maeneo yao mengine kuvamiwa na Wakaramojong kutoka Ethiopia.

Lugha yao inajulikana kama Kikadam, inafanana na Kiso, na ni sehemu ya kundi la lugha za Kinilo-Sahara. Lugha hiyo haitumiwi tena na vijana, hivyo inaelekea kufa[1].

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wakadam kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.