Yemen
Jamhuri ya Yemen ٱلْجُمْهُورِيَّةُ ٱلْيَمَنِيَّةُ (Arabic) | |
|---|---|
| Kaulimbiu: ٱللَّهُ، ٱلْوَطَنُ، ٱلثَوْرَةُ، ٱلْوَحْدَةُ (Arabic) "Mungu, Taifa, Mapinduzi, Umoja" | |
| Wimbo wa taifa: الجمهورية المتحدة (Arabic) "Jamhuri Iliyoungana" | |
| Mji mkuu na mkubwa | Sanaa |
| Lugha rasmi | Kiarabu[1] |
| Dini (2020) |
|
| Uraia | Myemeni |
| Serikali | Jamhuri ya nusu-urais ya muungano mmoja (serikali ya mpito) |
• Rais | Rashad al-Alimi |
• Waziri Mkuu | Shaea al-Zindani |
• Spika wa Baraza la Wawakilishi | Sultan al-Barakani |
• Spika wa Baraza la Shura | Ahmed Obaid Bin Dagher |
Muungano wa Yemen | |
• Muungano | 22 Mei 1990 |
• Katiba ya sasa | 16 Mei 1991 |
| Eneo | |
| • Jumla | km2 455,503[3] |
| • Maji (asilimia) | Kidogo sana |
| Idadi ya watu | |
| • Kadirio la 2023 | 32,684,503[4] |
| • Msongamano | 71.8/km2 |
| PLT (PPP) | Kadirio la 2025 |
| • Jumla | $69.960 bilioni[5] |
| • Kwa kila mtu | $1,670 |
| PLT (Kawaida) | Kadirio la 2025 |
| • Jumla | $17.400 bilioni |
| • Kwa kila mtu | $416 |
| HDI (2023) | 0.470[6] |
| Gini (2014) | 36.7[7] |
| Sarafu | Rial ya Yemeni (YER) |
| Majira ya saa | UTC+3 (AST) |
| Msimbo wa simu | +967 |
| Jina la kikoa | .ye |
Yemen (kwa Kiarabu: ٱلْيَمَن, al-Yaman), rasmi Jamhuri ya Yemen, ni nchi iliyoko kwenye ncha ya kusini-magharibi ya Rasi ya Uarabuni barani Asia. Inapakana na Saudi Arabia kaskazini, Oman mashariki, na imepakana na Ghuba ya Aden na Bahari ya Shamu kusini na magharibi. Yemen ina eneo la takriban kilomita za mraba 555,000 na idadi ya watu inayokadiriwa kuwa zaidi ya milioni 34. Mji wake mkuu ni Sana'a, ingawa serikali kwa sasa inaendesha shughuli nyingi kutoka mji wa muda wa Aden kutokana na hali ya kisiasa. Yemen ni mojawapo ya nchi zenye historia ndefu ya ustaarabu katika eneo la Kiarabu, ikiwa ni nyumbani kwa falme za kale kama Saba na Himyar.
Hata hivyo, katika karne ya sasa, nchi hii imekumbwa na migogoro ya kisiasa na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodhoofisha uchumi na hali ya kibinadamu.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Hadi mwaka 1990 palikuwa na nchi mbili za Yemen ya Kaskazini na Yemen ya Kusini.
Ile ya kaskazini ilikuwa Ufalme wa Yemen baada ya Imamu Yahya Muhamad wa kundi la Zaidiya kuvamia velayat ya Yemen ya milki ya Waturuki Waosmani (1 Novemba 1918). Baadaye ikawa Jamhuri kwa njia ya mapinduzi (1962).
Ile ya kusini ilikuwa sehemu koloni (Aden) na sehemu nchi lindwa (Hadramaut) ya Waingereza. Baada ya ukoloni kwisha ikawa mara moja Jamhuri (30 Novemba 1967).
Nchi hizo mbili ziliungana tarehe 22 Mei 1990, lakini uongozi ulizidisha ufisadi, na tangu mwaka 2011 hali ya siasa ni tata. Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinaendelea kwa misaada kutoka nchi za nje, hasa kutokana na uwepo wa makundi makubwa adui ya Wasuni na Washia.
Matokeo yake ni njaa kwa wakazi 17,000,000 kiasi kwamba Yemen imehesabika kuwa nchi inayohitaji zaidi misaada ya kibinadamu.
Demografia
[hariri | hariri chanzo]Kabila
[hariri | hariri chanzo]Wakazi wengi ni Waarabu wa makabila mbalimbali; wengine ni machotara wa Kiarabu-Kiafrika, Waajemi na Wazungu.
Lugha
[hariri | hariri chanzo]Lugha rasmi na ya kawaida ni Kiarabu.
Dini
[hariri | hariri chanzo]Upande wa dini, wananchi karibu wote (99%) ni Waislamu, wakiwemo Wasuni (60–65%) na Washia (35-40%). Waliobaki ni Wakristo, Wayahudi, Wahindu au hawana dini yote.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- http://www.yemen.gov.ye/ Ilihifadhiwa 13 Desemba 2020 kwenye Wayback Machine.
- (Kiarabu) Yemen Government official portal
- Yemen entry at The World Factbook
- Yemen katika Open Directory Project
- Yemen profile from the BBC News
- Wikimedia Atlas of Yemen
| Nchi na maeneo ya Asia |
|
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
| 1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
| Makala hii kuhusu maeneo ya Yemen bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Yemen kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
- ↑ "Yemen Constitution" (PDF).
- ↑ "Yemen". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2024-12-17. Iliwekwa mnamo 2026-03-18.
- ↑ "Yemen area".
- ↑ "Annual Statistical Health Report 2023". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2023-06-09. Iliwekwa mnamo 2026-03-17.
- ↑ "IMF data".
- ↑ "Human Development Report 2025".
- ↑ "World Bank GINI".
