Yemen

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Yemeni)
Yemen
Bendera
Nembo
Ramani ya {{{jina_kawaida}}} duniani
Ramani ya {{{jina_kawaida}}}
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
15°21′ N 12°24′ E
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
 • Eneo la ardhi{{{eneo_ardhi}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY

Yemen (Kiarabu: الجمهورية اليمنية ) ni nchi kusini mwa Bara Arabu.

Imepakana na Omani, Saudia na Bahari Hindi.

Nchi za karibu ng'ambo ya mlango wa bahari wa Bab el Mandeb ni Eritrea, Jibuti na Somalia.

Eneo lake ni pamoja na kisiwa cha Sokotra na visiwa 200 vingine.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Hadi mwaka 1990 palikuwa na nchi mbili za Yemen ya Kaskazini na Yemen ya Kusini.

Ile ya kaskazini ilikuwa Ufalme wa Yemen baada ya Imamu Yahya Muhamad wa kundi la Zaidiya kuvamia velayat ya Yemen ya milki ya Waturuki Waosmani (1 Novemba 1918). Baadaye ikawa Jamhuri kwa njia ya mapinduzi (1962).

Ile ya kusini ilikuwa sehemu koloni (Aden) na sehemu nchi lindwa (Hadramaut) ya Waingereza. Baada ya ukoloni kwisha ikawa mara moja Jamhuri (30 Novemba 1967).

Nchi hizo mbili ziliungana tarehe 22 Mei 1990, lakini uongozi ulizidisha ufisadi, na tangu mwaka 2011 hali ya siasa ni tata. Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinaendelea kwa misaada kutoka nchi za nje, hasa kutokana na uwepo wa makundi makubwa adui ya Wasuni na Washia.

Matokeo yake ni njaa kwa wakazi 17,000,000 kiasi kwamba Yemen imehesabika kuwa nchi inayohitaji zaidi misaada ya kibinadamu.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wengi ni Waarabu wa makabila mbalimbali; wengine ni machotara wa Kiarabu-Kiafrika, Waajemi na Wazungu.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kiarabu.

Upande wa dini, wananchi karibu wote (99%) ni Waislamu, wakiwemo Wasuni (60–65%) na Washia (35-40%). Waliobaki ni Wakristo, Wayahudi, Wahindu au hawana dini yote.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Yemen bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Yemen kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.