Mkutano wa Lambeth

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Lambeth Conference au Mkutano wa Lambeth ni mkutano wa maaskofu wa Jumuiya Anglikana unaoitishwa na Askofu Mkuu wa Canterbury kila baada ya miaka 10. Mkutano kama huo wa kwanza ulifanyika huko Lambeth, Uingereza mnamo mwaka 1867.

Kwa kuwa Jumiya Anglikana ni umoja wa kimataifa wa makanisa yanayojitawala, mkutano huo hauna mamlaka ya kiutawala.

Mikutano ya Lambeth hufanya kazi ya kushirikiana na kushauriana, ikionyesha "nia ya jumuiya" katika ya masuala ya siku. [1]

Maazimio ya Mkutano wa Lambeth yanayayopitishwa nao hayana athari za kisheria, hata hivyo yana ushawishi. Kwa hiyo, ingawa maazimio ya mikutano hayana mamlaka ya kisheria, "yanabeba mamlaka kubwa ya maadili na kiroho."  "Matamshi yake juu ya masuala ya kijamii yameathiri sera katika makanisa."

Katika karne ya 21 Mkutano wa Lambeth umeingia katika kipindi kigumu. Ndani ya Jumuiya Anglikana zimetokea tofauti kali kuhusu masuala ya maadili, hasa suala la kukubali wanawake kubarikiwa kuwa makasisi na maaskofu, suala la kubariki ndoa ya jinsia moja na suala la makasisi wanaoishi kaika ndoa za jinsia moja. Masuala hayo yamefanya maaskofu kadhaa kukataa kuhudhuria tena mikutano. Kwenye mkutano wa Lambeth wa mwaka 2008 robo moja ya maaskofu wote ilikataa kufika baada ya kubarikiwa kuwa askofu kasisi aliyeishi katika ndoa ya jinsia moja. Hapo Askofu Mkuu wa Canterbury aliamua kutoitisha mkutano wa mwaka 2018[2]. Mkutano wa maaskofu wakuu wa majimbo uliazimia kuwa na mkutano wa Lambeth kwenye mwaka 2020 lakini ukaahirishwa tena shauri ya mlipuko wa virusi vya Corona hadi 2022[3].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. The truth shall make you free: the Lambeth Conference 1988: the reports, resolutions & pastoral letters from the bishops (Church House Publishing, 1988), p. 118
  2. Kevin Kallsen: Lambeth Conference cancelled. 30 Septemba 2014, iliangaliwa 13 Julai 2020.
  3. |titel=Welcome to official web site of the fifteenth Lambeth Conference 27 July – 8th August 2022

Bibliografia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]