Mbwa Mkubwa (kundinyota)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyota za Mbwa Mkubwa (Canis Major) katika mazingira yao angani
Ramani ya kundinyota Mbwa Mkubwa (Canis Maior) jinsi inavyoonekana kwa mtazamaji kwenye nusutufe ya kaskazini ya Dunia

Mbwa Mkubwa (kwa Kilatini na Kiingereza Canis Maior) [1] ni jina la kundinyota kwenye angakusi ya Dunia yetu. Shira (Sirius) ambayo ni nyota angavu zaidi angani ni sehemu ya Mbwa Mkubwa.

Mahali pake

Mbwa Mkubwa lipo karibu na kundinyota la Jabari (en:Orion) kwa upande wa kusini ya ikweta ya anga. Sehemu yake ya mashariki inafika kwenye Njia Nyeupe. Makundinyota jirani yake ni Arinabu (Lepus au sungura), Munukero (kundinyota) (Monocerus), Shetri (Puppis) na Njiwa (kundinyota) (Columba).

Jina

Mbwa Mkubwa lilijulikana kwa jina hili kwa miaka mingi kati ya mabaharia Waswahili waliotumia nyota kutafuta njia baharini wakati wa usiku.[2]

Jina "Mbwa Mkubwa" linatokana na mitholojia ya Ugiriki ya Kale iliyoona hapa mbwa anayewinda pamoja na Jabari (Orion) na kumfuata Akarabu (sungura). Baadaye mbwa wa pili alibuniwa na Waroma. [3] na hapo makundinyota hayo mawili yaliitwa Mbwa Mkubwa na Mdogo. Majina haya yalitafsiriwa baadaye moja kwa moja kwa Kilatini kuwa Canis Maior na Minor na baadaye kwa Kiarabu kuwa الكلب الأكبر al-kalb al-ʾakbar (Mkubwa) na الأصغر al-ʾaṣghar (Mdogo).

Mbwa Mkubwa ni kati ya makundinyota yaliyotajwa tayari na Klaudio Ptolemaio katika karne ya 2 BK. Iko pia katika orodha ya makundinyota 88 ya Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [4] kwa jina la Canis Maior. Kifupi chake rasmi ni 'CMa'.[5]

Nyota

Nyota angavu zaidi ni Shira (α Alfa Canis Maioris) inayojulikana pia kwa jina la kimataifa ya en:Sirius. Hii pia ni nyota angavu zaidi kushinda nyota zote kwenye anga ikiwa na mwangaza unaoonekana wa -1.4 mag na umbali wake na dunia ni miakanuru 8.6 (parseki 2.64)

Jina la
(Bayer)
Namba ya
Flamsteed
Jina
(Ukia)
Mwangaza
unaoonekana
Umbali
(miaka nuru)
Aina ya spektra
α 9 Shira (Sirius) −1,5m 8,7 A1 V
ε 21 Adhara 1,50m 431 B2 III
δ 25 Wezen 1,83m 1600 F8 Ia
β 2 Mirzam 1,98m 715 B1 II
η 31 Aludra 2,45m 3200 B5 Ia
ζ 1 Furud 3,02m 330
ο2 24 3,02m 2500 B3 Ia
σ 22 3,49m 1500 K8 Ib
ο1 16 3,89m 2000 K3 Ia
ν2 7 3,95m 80 K1 III
ω 28 4,01m 500 B3 IV

Tanbihi

  1. Uhusika milikishi (en:genitive) ya neno "Canis Maior" katika lugha ya Kilatini ni " Canis Maioris " na hili ni umbo la jina linaloonekana katika majina ya nyota za kundi hili kama vile Alfa Canis Maioris, nk.
  2. ling. Knappert 1993
  3. ling. Allen, Star-Names and their Meanings uk, 117
  4. The Constellations, tovuti ya International Astronomical Union , iliangaliwa Julai 2017
  5. Russell, Henry Norris (1922). "The New International Symbols for the Constellations". Popular Astronomy 30: 469–71. Bibcode:1922PA.....30..469R. 

Marejeo

Marejeo

  • Richard Hinckley Allen: Star-Names and their Meanings; kwa G. E. Stechert New York, Leipzig, London, Paris 1899, ukurasa 75 ff (online hapa kwenye archive.org)
  • Jan Knappert, 1993: The Swahili Names of Stars, Planets and Constellations; The Indian Ocean Review September 1993 Volume 6 No. 3 September 1993, kurasa 6-7, ISSN 1031-2331
Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mbwa Mkubwa (kundinyota) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.