Njiwa (kundinyota)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyota za kundinyota Njiwa (Columba) katika sehemu yao ya angani

Njiwa (kwa Kilatini na Kiingereza Columba) [1]. miakanurua kundinyota kwenye nusutufe ya kusini ya dunia yetu. Lipo jirani na kundinyota la Mbwa Mkubwa na Mkuku (lat. Carina).

Jina[hariri | hariri chanzo]

Njiwa linapatikana kati ya makundinyota yaliyobuniwa tangu mabaharia Wazungu walipozunguka Dunia yote katika karne ya 16 na kuona mara ya kwanza nyota ya kusini na wachoraji wa ramani kukamilisha atlasi za nyota. Mnamo mwaka 1612 Mholanzi Petrus Plancius alitenga nyota hizi kutoka kundinyota la Mbwa Mkubwa [2] na kuzitaja "Njiwa" kwa kumbukumbu ya njiwa iliyetumwa na Nuhu katika masimulizi ya Biblia [3] na kuzichora hivyo katika globu ya nyota yake. Kifupi chake rasmi kufuatana na Ukia ni Col[4].

Nyota[hariri | hariri chanzo]

Nyota angavu zaidi ni Phact au Alpha Columbae yenye mwangaza unaoonekana wa mag 2.7. Hii ni nyota yenye rangi ya buluu-nyeupe iliyo na umbali wa miaka nuru 268 kutoka kwetu duniani.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Uhusika milikishi (en:genitive) ya neno "Columba" katika lugha ya Kilatini ni " Columbae" na hili ni umbo la jina linaloonekana katika majina ya nyota za kundi hili kama vile Alfa Columbae, nk.
  2. http://www.ianridpath.com/startales/columba.htm Ian Ridpath's Star Tales: Columba, the Dove
  3. ling. Kitabu cha Mwanzo 8, 8-12
  4. Tovuti ya Ukia, The Constellations, iliangaliwa Septemba 2017