Alma Redemptoris Mater

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Madonna kadiri ya Raffaello Sanzio.
Alma Redemptoris Mater kwa muziki wa fahari.

"Alma Redemptoris Mater" (tamka: ˈalma redempˈtoris ˈmater; maana yake: 'Mpendwa Mama wa Mkombozi') ni utenzi wa Kikristo unaotumika katika liturujia ya Kanisa la Kilatini hasa kama antifona mojawapo ya kumalizia Sala ya mwisho nje ya Kipindi cha Pasaka.

Utenzi huo ulitungwa na Hermannus Contractus (1013–1054) kwa kutegemea maandishi ya Fulgensyo wa Ruspe, Epifani wa Salamina na Irenei wa Lyon.[1].

Maneno asili kwa Kilatini[hariri | hariri chanzo]

Alma Redemptóris Mater, quæ pérvia cæli
Porta manes, et stella maris, succúrre cadénti,
Súrgere qui curat pópulo: tu quæ genuísti,
Natúra miránte, tuum sanctum Genitórem
Virgo prius ac postérius, Gabriélis ab ore
Sumens illud Ave, peccatórum miserére.

[2]

Tafsiri huru ya Kiswahili[hariri | hariri chanzo]

Ewe Mama wa Kristo, sikia kilio chetu,
Ewe nyota ya bahari, ewe Mlango wa mbingu,
Mama wa yeye mwenyewe, ambaye alikuumba,
Tunapozama topeni, msaada twakuomba;
Kwa furaha ile ile, Gabrieli alokupa,
E Bikira wa pekee, wa kwanza na mwisho pia,
Twakuomba utujalie, tupewe yako huruma.

[3]

Muziki wake[hariri | hariri chanzo]

Utenzi huo ulipambwa kwa muziki na Marc-Antoine Charpentier.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. : The Tradition of Catholic Prayer by Christian Raab, Harry Hagan 2007 ISBN 0-8146-3184-3 page 234
  2. Handbook of Prayers by James Socías 2006 ISBN|0-87973-579-1 page 472
  3. "Sala ya Kanisa", BPNP, uk. 1236.