Nenda kwa yaliyomo

Mama wa Mungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Theotokos)
Katika nakshi hii iliyopo kwenye Basilika la Hagia Sofia, huko Istanbul herufi za Kigiriki ΜΡ ΘΥ zinamaanisha Mama wa Mungu.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Yesu
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho   Utoto wa Yesu   Ubatizo   Arusi ya Kana   Utume wa Yesu   Mifano ya Yesu   Miujiza ya Yesu   Kugeuka sura   Karamu ya mwisho   Msalaba wa Yesu   Maneno saba   Kifo cha Yesu   Ufufuko wa Yesu   Kupaa mbinguni   Ujio wa pili  Yesu na matabiri ya Agano la Kale   Injili   Majina ya Yesu katika Agano Jipya   Yesu kadiri ya historia   Tarehe za maisha ya Yesu   Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi   Kiaramu   Bikira Maria   Yosefu (mume wa Maria)   Familia takatifu   Ukoo wa Yesu   Ndugu wa Yesu   Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya  · Mitazamo ya Kikristo   Mitazamo ya Kiyahudi   Mitazamo ya Kiislamu   Yesu katika sanaa

Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki

Mama wa Mungu (kwa Kigiriki Θεοτόκος, Theotókos; kwa Kilatini Deipara au Dei genetrix, yaani "Mzaa Mungu") ni sifa kuu ambayo Wakristo wengi wanampatia Bikira Maria mama wa Yesu Kristo.

Msingi wa imani hiyo

[hariri | hariri chanzo]

Kwa kuwa wafuasi wa Yesu wanasadiki kuwa yeye ni Mungu sawa na Baba, wengi wao wanakubali kuwa aliyemzaa kama binadamu anastahili kuitwa Mama wa Mungu.

Sifa hiyo ilianza kutumika katika karne ya 2, labda nchini Misri, ikathibitishwa moja kwa moja na Mtaguso wa Efeso (431) dhidi ya Patriarki Nestori aliyedai anaweza kuitwa tu Mama wa Yesu au Mama wa Kristo.

Mtaguso mkuu huo uliona kwamba Nestori alimgawa Yesu katika nafsi mbili: ya Kimungu na ya kibinadamu. Kumbe imani sahihi inamkiri kwamba nafsi ya Yesu ni ile ya Kimungu tu ambayo ni ya pili katika Utatu Mtakatifu. Hivyo aliyemzaa Yesu kama binadamu (si kama Mungu, jambo ambalo haliwezekani) anastahili kuitwa Mama wa Mungu (upande wa ubinadamu wake alioutwaa kwake).

Heshima katika sala

[hariri | hariri chanzo]

Kwa namna ya pekee, Maria anapewa sifa hiyo katika sala ya Salamu Maria, iliyo maarufu zaidi kati ya sala za Ukristo wa magharibi kwa mama wa Yesu.

Adhimisho katika liturujia

[hariri | hariri chanzo]

Sikukuu yake inaadhimishwa na Wakatoliki wanaofuata mapokeo ya Kanisa la Roma tarehe 1 Januari, siku ya nane (Oktava) ya Noeli, lakini Wakatoliki wengine wanaiadhimisha siku tofauti, kwa mfano huko Milano ni Jumapili kabla ya Noeli.

Marejeo ya Kiswahili

[hariri | hariri chanzo]
  • Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 7-9
  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk 1-2
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 1-2

Marejeo ya lugha nyingine

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mama wa Mungu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.