Mama wa Kanisa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mozaiki Mater Ecclesiae katika uwanja wa Basilika la Mt. Petro.

Mama wa Kanisa (kwa Kilatini: Mater Ecclesiae) ni jina la heshima ambalo Bikira Maria amepewa rasmi na Papa Paulo VI tarehe 21 Novemba 1964 wakati wa Mtaguso wa pili wa Vatikano. Jina hilo lilitumiwa kwanza na Ambrosi wa Milano katika karne ya 4[1] halafu na Papa Benedikto XIV mwaka 1748[2], tena na Papa Leo XIII mwaka 1885.[3]

Limeingizwa na Papa Yohane Paulo II katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki[4], hatimaye na Papa Fransisko katika kalenda ya liturujia ya Kanisa la Kilatini siku inayofuata Pentekoste.[5]

Kabla ya hayo yote, sanaa ya Kikristo ilikuwa imezoea kumchora Bikira Maria kati ya Mitume wakati wa kushukiwa na Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste kama ilivyosimuliwa na Mwinjili Luka (Mdo 1-2).

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Hugo Rahner, "Mater Ecclesia - Lobpreis der Kirche aus dem ersten Jahrtausend", Einsiedeln/Köln 1944
  2. Bullarium Romanum,series 2, t. 2, n. 61, p. 428
  3. Acta Leonis XIII, 15, 302
  4. "Mary, Mother of Christ, Mother of the Church." Catechism item 963 at the Vatican web site
  5. "Decreto della Congregazione per il Culto Divino e la Disciplina dei Sacramenti sulla celebrazione della beata Vergine Maria Madre della Chiesa nel Calendario Romano Generale". press.vatican.va. Iliwekwa mnamo 2020-07-01. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: