Msaada wa Wakristo
Mandhari


Msaada wa Wakristo (kwa Kilatini: Auxilium Christianorum) ni sifa mojawapo ya Bikira Maria katika Kanisa Katoliki.
Yohane Krisostomo alikuwa wa kwanza kutumia jina hilo mwaka 345.
Baadaye, Ukristo ulipoatharishwa na uenezi wa Waislamu, waumini walimkimbilia Maria kwa jina hilo ili kupata msaada wa sala zake. Hasa mwaka 1571, Waturuki walipokaribia kuteka Ulaya, Papa Pius V aliombea jeshi la Kikristo kwa kuagiza sala ya Rozari hadi ushindi ulipopatikana katika mapigano ya Lepanto.
Yohane Bosco ndiye aliyeeneza zaidi heshima hiyo.
Mtaguso wa pili wa Vatikano, katika hati juu ya Kanisa (61, 62), ulitaja jina hilo ukieleza umama wa Maria[1].
Katika sanaa
[hariri | hariri chanzo]- Sanamu huko Miguel Hidalgo, Federal District, Mexico
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "In an utterly singular way she co-operated by her obedience, faith, hope and burning charity in the Saviour's work of restoring supernatural life to souls. For this reason she is a mother to us in the order of grace…By her maternal charity, Mary cares for the brethren of her Son who still wander through this world in the midst of dangers and difficulties until they are led to the happiness of their heavenly home". Daniel, Michael. "Our Lady Help of Christians"
- ↑ Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 146
