Nyota ya bahari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Bibi Yetu Nyota ya Bahari, Sliema, Malta.

Nyota ya bahari (kwa Kilatini: Stella Maris) ni sifa mojawapo iliyotumika kwa Bikira Maria tangu mwanzoni mwa Karne za Kati.

Kwa jina hilo anaheshimiwa na kukimbiliwa na mabaharia Wakatoliki katika hatari za safari majini.