Bahari ya Amundsen

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu ya Bahari ya Amundsen katika Antaktiki.
Bahari zinazopakana na Antaktiki.
Siwabarafu latika Bahari ya Amundsen.

Bahari ya Amundsen ni mkono wa Bahari ya Kusini upande wa magharibi wa Bara la Antaktiki kwenye eneo la longitudo ya 110°[1]. Upande wa mashariki inapakana na Bahari ya Bellingshausen, upande wa magharibi hakuna sehemu ya bahari iliyopewa jina maalumu, hadi Bahari ya Ross kwa umbali wa km 1,000.[2]

Bahari imefunikwa na barafu kwa muda mrefu wa mwaka. Barafuto inayosukuma barafu baharini ina unene wa kilomita 3 na eneo lake ni kilomita za mraba 700,000.

Bahari hiyo imepewa jina lake kwa heshima ya Roald Amundsen, mpelelezi wa ncha za Dunia kutoka nchini Norwei, aliyekuwa binadamu wa kwanza aliyefaulu kufika kwenye ncha ya kusini. Kwa miaka mingi mstari wa pwani haukujulikana kwa sababu unene wa barafu hauonyeshi tofauti kati ya bahari na nchi kavu. Tangu mwaka 1940 Mwamerika Richard Evelyn Byrd alifanya utafiti kwa msaada wa eropleni akaweza kutambua pwani.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Australian Antarctic Data Centre: Amundsen Sea
  2. Andrew Jon Hund (Hrsg.): Antarctica and the Arctic Circle: A Geographic Encyclopedia of the Earth's Polar Regions: Amundsen Sea. ABC-Clio, Santa Barbara 2014, ISBN 978-1-61069-392-9.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.