Bahari ya Kara

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Bahari ya Kara.

Bahari ya Kara ni tawi la Bahari ya Aktiki, kaskazini kwa Urusi. Eneo lake la km² 893.400 liko baina ya visiwa vya Novaya Semlya na Severnaya Semlya.

Bahari ya Kara inapokea maji ya mito mikubwa ya Yenisei na Ob.

Kutokana na tabianchi baridi uso wa bahari hii huganda ukifunikwa na barafu kwa takriban miezi 9 kila mwaka.

Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.