Bahari ya Tyrrheni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bahari ya Tireni)
Bahari ya Tyrrheni

Bahari ya Tyrrheni (kwa Kiingereza Tyrrhenian Sea; kwa Kiitalia: Mar Tirreno) ni sehemu ya Bahari Mediteranea.

Iko kati ya rasi ya Italia upande wa mashariki na visiwa vya Korsika, Sardinia na Sisilia upande wa magharibi na kusini.

Jina linatokana na jinsi Wagiriki wa Kale walivyoiita nchi ya Waetruski waliokalia pwani za Italia magharibi.

Bandari muhimu ni Naples, Palermo, Civitavecchia (Roma), Salerno, Trapani mbali ya Bastia kwenye kisiwa cha Korsika.

Makala hii kuhusu maeneo ya Italia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bahari ya Tyrrheni kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.