Ghuba ya Alaska

Majiranukta: 57°N 144°W / 57°N 144°W / 57; -144
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Ghuba ya Alaska
Ramani ya Ghuba ya Alaska

Ghuba ya Alaska (kwa Kiingereza: Gulf of Alaska) ni mkono wa Bahari Pasifiki. Inapakana na pwani ya kusini ya Alaska. Inaenea baina ya kisiwa cha Kodiak upande wa magharibi hadi funguvisiwa la Aleksander upande wa mashariki.

Pwani yake inapindapinda sana kutokana na hori nyingi na mikonobahari inayoingia ndani ya nchi kavu. Pwani huwa na misitu, milima na barafuto nyingi.

Hori ya Lituya ni mahali ambako ilitokea tsunami kubwa inayojulikana duniani kwenye mwaka 1958, wimbi lake lilipita kimo cha mita 500[1].

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Giant Waves in Lituya Bay, Alaska; USGS PP 354-C, tovuti ya uwsp.edu jinsi ilivyohifadhiwa kwenye archive.org, iliangaliwa Septemba 2019

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

57°N 144°W / 57°N 144°W / 57; -144