Bahari ya Labrador

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Bahari ya Labrador
Nyangumi na siwa barafu katika Bahari ya Labrador

Bahari ya Labrador (kwa Kiingereza: Labrador Sea, kwa Kifaransa: mer du Labrador) ni mkono wa Bahari Atlantiki uliopo baina ya rasi ya Labrador na Greenland. Upande wa kaskazini unaendelea katika Hori ya Baffin kupitia Mlangobahari wa Davis.[1] Imeitwa pia bahari ya pembeni (en:marginal sea ya Atlantiki.[2][3]

Kina cha Bahari ya Labrador kinafikia mita 3400 kwenye kusini inapounganishwa na Atlantiki; katika sehemu hii ina upana wa km 1,000. Upande wa kaskazini kina hupungua hadi mita 700 ikipita kwenye mlangobahari wa Davis.[4]

Halijoto ya maji haipandi juu ya sentigredi 5-6 na wakati wa baridi theluthi mbili za uso wake zinaganda kuwa barafu.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Encyclopædia Britannica. Labrador Sea. Iliwekwa mnamo 2008-02-03.
  2. Peter Calow (12 July 1999). Blackwell's concise encyclopedia of environmental management. Wiley-Blackwell. p. 7. ISBN 978-0-632-04951-6. Retrieved 29 November 2010. 
  3. Boundary Currents and Watermass Transformation in Marginal Seas
  4. Wilson, R. C. L; London, Geological Society of (2001). "Non-volcanic rifting of continental margins: a comparison of evidence from land and sea". Geological Society, London, Special Publications 187: 77. ISBN 978-1-86239-091-1. doi:10.1144/GSL.SP.2001.187.01.05. 

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons


Coordinates: 61°N 56°W / 61°N 56°W / 61; -56 (Labrador Sea)