Bahari ya Labrador


Bahari ya Labrador (kwa Kiingereza: Labrador Sea, kwa Kifaransa: mer du Labrador) ni mkono wa Bahari Atlantiki uliopo baina ya rasi ya Labrador na Greenland. Upande wa kaskazini unaendelea katika Hori ya Baffin kupitia Mlangobahari wa Davis.[1] Imeitwa pia bahari ya pembeni (en:marginal sea ya Atlantiki.[2][3]
Kina cha Bahari ya Labrador kinafikia mita 3400 kwenye kusini inapounganishwa na Atlantiki; katika sehemu hii ina upana wa km 1,000. Upande wa kaskazini kina hupungua hadi mita 700 ikipita kwenye mlangobahari wa Davis.[4]
Halijoto ya maji haipandi juu ya sentigredi 5-6 na wakati wa baridi theluthi mbili za uso wake zinaganda kuwa barafu.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Encyclopædia Britannica. Labrador Sea. Iliwekwa mnamo 2008-02-03.
- ↑ Peter Calow (12 July 1999). Blackwell's concise encyclopedia of environmental management. Wiley-Blackwell, 7. ISBN 978-0-632-04951-6. Retrieved on 29 November 2010.
- ↑ Boundary Currents and Watermass Transformation in Marginal Seas
- ↑ Wilson, R. C. L; London, Geological Society of (2001). "Non-volcanic rifting of continental margins: a comparison of evidence from land and sea". Geological Society, London, Special Publications 187: 77. . . https://books.google.com/books?id=-bsvkxVBTasC&pg=PA77.