Jimbo Katoliki la Same
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jimbo Katoliki la Same (kwa Kilatini Dioecesis Samensis) ni mojawapo kati ya majimbo 33 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania, na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Kiroma.
Kanisa kuu liko mjini Same, katika mkoa wa Kilamanjaro na limewekwa wakfu kwa heshima ya Kristo mfalme.
Linahusiana na Jimbo Kuu la Arusha.
Yaliyomo |
Takwimu [hariri]
Eneo lake lote ni kama kilometa mraba 10,000, ambamo wamo wakazi 562,950. Kati yao Wakatoliki ni 70,490 (2004) yaani asilimia 12.5.
Waamini hawa wanahudumiwa na mapadri 40, ambao kati yao 35 ni wanajimbo na 5 watawa. Hivyo kwa wastani kila mmojawao anahudumia waamini 1.762.
Parokia ziko 62.
Jimbo lina mabruda 13 na masista 40.
Historia [hariri]
- 10 Desemba 1963: Kuanzishwa kwa Apostolic Prefecture ya Same kutokana na Jimbo Katoliki la Moshi
- 3 Februari 1977: Kufanywa jimbo kamili
Uongozi [hariri]
- Apostolic Prefect
- Maaskofu
- Josaphat Louis Lebulu (12 Februari 1979 - 28 Novemba 1998 kufanywa askofu mkuu wa Jimbo Kuu la Arusha)
- Jacob Venance Koda (16 Machi 1999 - 15 Aprili 2010 kujiuzulu)
- Rogatus Kimaryo, C.S.Sp. (30 Aprili 2010 - )
Viungo vya nje [hariri]
- Giga-Catholic Information
- Catholic Hierarchy
- Hati Adpetens Natalis Christi
- Hati Praefecturam illam, AAS 69 (1977), uk. 318