Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro |
|
Mahali pa Mkoa wa Morogoro katika Tanzania | |
Majiranukta: 8°0′S 37°0′E / 8.000°S 37.000°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Wilaya | 6 |
Mji mkuu | Morogoro |
Serikali | |
- Mkuu wa Mkoa | Issa Machibya |
Eneo | |
- Jumla | 73,039 km² |
Idadi ya wakazi (2002) | |
- Wakazi kwa ujumla | 1,759,809 |
Tovuti: http://www.morogoro.go.tz/ |
Morogoro ni jina la mji, wilaya na mkoa wa Tanzania.
Mkoa wa Morogoro ni kati ya mikoa 26 ya Tanzania. Umepakana na mikoa ya Tanga, Pwani, Lindi, Ruvuma, Iringa, Dodoma na Arusha. Ikiwa eneo lake ni 72 939 km² kuna wakazi 1,759,809 (mwaka 2002). Morogoro iko kati ya mikoa mikubwa zaidi ya Tanzania.
Utawala
Mkoa una wilaya sita ndizo (idadi ya wakazi kwa mabano): Kilosa ( 489,513), Kilombero (322,779), Morogoro Vijijini (263,920), Morogoro Mjini (228,863), Mvomero (260,525), Ulanga (194,209). Wakazi walio wengi hukalia wilaya za kaskazini mkoani. Robo yao huishi katika miji ya mkoa.
Ramani | Wilaya au manisipaa | Wakazi (2002) | Tarafa | Kata | Kijiji | Eneo km² |
---|---|---|---|---|---|---|
Wilaya ya Kilombero | 321,611 | 5 | 19 | 81 | 14,918 | |
Wilaya ya Kilosa | 489,513 | 9 | 37 | 164 | 14,245 | |
Wilaya ya Morogoro Vijijini | 263,920 | 6 | 25 | 132 | 11,925 | |
Wilaya ya Morogoro Mjini | 227,921 | 1 | 19 | - | 531 | |
Wilaya ya Mvomero | 260,525 | 4 | 17 | 101 | 7,325 | |
Wilaya ya Ulanga | 193,280 | 5 | 24 | 65 | 24,560 | |
Jumla | 1,759,809 | 30 | 141 | 543 | 73,039 | |
Makisio ya idadi ya watu kwa mwaka 2008 ni watu 2,021,714 kutokana na kiwango cha ongezeko la watu la asilimia 2.6 kwa mwaka. | ||||||
Marejeo: Mkoa wa Morogoro |
Eneo
Eneo la Mkoa wa Morogoro liko katikati ya mikoa ya pwani la Bahari Hindi na Nyanda za Juu. Kuna tambarare za chini kama vile Ifakara / Kilombero pia milima ya juu kama Uluguru penye mlima wa Kimhandu mwenye 2646 m juu ya UB.
Mito mikubwa ni Wami na Ruvu inayoanza kwenye milima ya Uluguru. Ruvu ndiyo mto wa kutoa maji ya Daressalaam.
Karibu nusu ya eneo la Mkoa wa Morogoro ni hifadhi za wanyama za Mikumi, Udzungwa na Selous.
Wakazi
Kabila kubwa ni Waluguru waliotoa jina kwa mji wa Morogoro pamoja na milima ya Uluguru. Makabila mengine makubwa zaidi ni Wangulu, Wakagulu, Wasagala na Wapogolo.
Mawasiliano
Barabara Kuu za lami za Daressalaam - Morogoro - Mbeya - Zambia/Malawi na Daressalaam - Morogoro - Dodoma hupita eneo la mkoa pamoja na reli ya kati Daresalaam - Morogoro - Dodoma - Kigoma / Mwanza. Reli ya TAZARA hupita wilaya ya Kilombero.
Uchumi
Kilimo kinategemea hali ya mvua. Kilombero kuna mashamba makubwa ya miwa. Mazao ya sokoni hulimwa milimani. Katibu nusu ya eneo la mashamba yote hulimwa mahindi.
Marejeo ya Nje
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Songwe | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |