Madagaska

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Repoblikan'i Madagasikara
Republique de Madagascar
Jamhuri ya Madagaska
Bendera ya Madagaska. Nembo ya Madagaska.
(Bendera ya Madagaska) (Nembo ya Madagaska)
Wimbo wa Taifa: Tanindrazana, Fahafahana, Fandrosoana
(kwa Kimalagasi: Nchi ya wenyeji, Uhuru, Maendeleo) |
Mahali pa Madagaska.
Lugha rasmi Kimalagasi
Kifaransa
Mji Mkuu Antananarivo
Rais
Waziri Mkuu
Andry Rajoelina
Christian Ntsay
Eneo
 - Jumla
 - 0.9% Maji
Ya 46 duniani
km² 587,041
Umma
 - Kadirio (Ya 52 duniani)
 - Jumla (26,262,313 )
 - Umma kugawa na Eneo 35.2
Ya 174 duniani
; (Ya 142 duniani)
GDP Chumo cha uchumi
 - Jumla
 - kwa kipimo cha umma
126 kadir
$15.82 billion (223)
$900 (214)
Uhuru
26 Juni 1960
Fedha Ariari
Saa za Eneo UTC +3
Wimbo wa Taifa Ry Tanindraza nay malala ô (Eh, nchi yetu asili) |
Intaneti TLD .mg
kodi za simu 261
1Lugha ya Malagasi, kulingana na katiba ndiyo lugha ya Taifa. Lugha ya Kifaransa, haijatiwa umaakini kama Lugha rasmi.
Ramani ya Madagaska.

Jamhuri ya Madagaska (au Madagasikari) inaenea katika kisiwa cha Madagaska (pia: Bukini) kilichopo katika Bahari Hindi mashariki kwa pwani ya Afrika.

Jina[hariri | hariri chanzo]

Jina Madagaska lina maana ya "Kisiwa kikubwa" na linatokana na lugha ya wenyeji, Wamalagasi ambao waongea Kimalagasi.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Kisiwa chenyewe ni cha nne kwa ukubwa duniani.

Upekee wa kisiwa unatokana na kwamba kilimeguka kutoka India miaka milioni 88 hivi iliyopita, halafu kilibaki bila watu hadi karne ya 5 hivi BK.

Ekolojia[hariri | hariri chanzo]

Kisiwa hicho ni pia mazingira makubwa ya aina ya violezo ambayo ni asilimia 5 ya violezo vyote vya mimea na wanyama vya dunia nzima.

Asilimia 90 ya viumbehai asili ni maalumu wa Madagaska, kama vile wanyama aina ya kima awali wanaoitwa lemuri, ndege ambao waambukiza ugonjwa na mti wa mbuyu.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mfalme Andrianampoinimerina (1787-1810).
Bendera ya Ufalme wa Merina.
Nembo ya Ufalme wa Merina.

Madagaska ni kati ya maeneo ya mwisho kufikiwa na kukaliwa na binadamu.

Wa kwanza kufika walitokea visiwa vya Indonesia (kama mwaka 350-550 BK).

Baadaye tu walihamia watu kutoka bara la Afrika (mwaka 1000 hivi) na wengineo (Waarabu, Wahindi, Wazungu, Wachina n.k.).

Kuanzia mwaka 1787 hadi mwaka 1897 kisiwa kilizidi kuunganishwa kisiasa chini ya Ufalme wa Merina.

Watawala walikuwa watu kutoka familia ya Andrianampoinimerina, mwanzilishi wa taifa hilo, ambaye alikuwa ametokea katika kabila la Wamerina

Kabila hilo lilikuwa kubwa na muhimu kuliko yote 18 ya kisiwa hicho. Makazi yake yalikuwa katika uwanda wa juu wa kati lakini lilienea sehemu kubwa ya Bukini.

Wamerina walikuwa na makao makuu ya utawala wao Antananarivo; baada ya kugawiwa kwa ufalme wao mnamo 1710 kitovu cha malaka kati ya Wamerina ikahamia kwenye mlima wa Ambohimanga lakini tangu kuunganishwa kwa Wamerina mnamo 1794 mji mkuu ukulikuwa tena Atananarivo. Kutoka hapo waliweza kueneza mamlaka yao katika sehemu nyingine za kisiwa hicho.

Makabila yote ya wenyeji yalizungumza lugha moja na yalikuwa na mila na desturi zinazofanana, hivyo yaliweza kujenga umoja wa kiutamaduni uliowafanya wawe jamii moja kimsingi.

Watawala hao wa kifalme waliweza kutekeleza mambo mbalimbali kuendeleza Bukini katika vipindi vyao kabla ya kuja kwa wageni kutoka Uingereza na Ufaransa ambao kwa kiasi fulani ulidhoofisha mamlaka ya kifalme.

Kisiwa hicho hatimaye kiligeuzwa kuwa koloni la Ufaransa. Hii ni kwa kuwa, ingawa sera ya kuisasisha ya Bukini kwa namna fulani iliimarisha uwezo wa nchi hiyo wa kutetea uhuru wake, lakini kwa ujumla sera hiyo ilidhoofisha ufalme huo kwa kuongeza utegemezi wake kwa mataifa ya kigeni.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Mtoto wa Kimalagasi anayeonyesha kuwa na mchanganyiko wa damu.

Mwaka 2018 idadi ya wakazi ilikadiriwa kuwa milioni 26.3. Wenyeji wengi wana mchanganyiko wa damu: DNA inaonyesha kuwa wakazi wa kwanza kutoka Indonesia wameichangia asilimia 50 hivi na Waafrika vilevile. Wanaoishi sehemu za ndani ni wa Kiindonesia zaidi, wakati wale wa pwani ni wa Kiafrika zaidi.

Lugha[hariri | hariri chanzo]

Lugha ya taifa ni Kimalagasi. Lugha rasmi za Madagaska ni Kimalagasi na Kifaransa (angalia pia orodha ya lugha za Madagaska).

Dini[hariri | hariri chanzo]

Mwaka 1993 nchini Madagaska kulikuwa na dini za jadi (52% hivi), Ukristo (41%, Waprotestanti wakiwazidi kidogo Wakatoliki), Uislamu (7% hivi) n.k. Tangu hapo wafuasi wengi wa dini za jadi wameongokea Ukristo, hasa wa Kiprotestanti.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Pamoja na kutokea mazingira tofauti sana, Wamalagasi wamechanganyikana sana na kuwa na utamaduni na lugha aina moja, ya Kiindonesia zaidi.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

      . http://books.google.com/books?id=Szvr5hUtD5kC&printsec=frontcover.
      .
      . http://books.google.com/books?id=3mE04D9PMpAC&printsec=frontcover.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Coordinates: 20°S 47°E / 20°S 47°E / -20; 47

Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Madagaska kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.