Kima
| Kima | ||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kima buluu
|
||||||||||||||
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
|
||||||||||||||
| Ngazi za chini | ||||||||||||||
|
Catarrhini (Kima wa Dunia ya Kale) |
Kima ni mamalia yeyote wa hali ya juu katika makundi ya cercopithecoid (kima wa Dunia ya Kale) au "platyrrhine" (Kima wa Dunia Mpya). Mamalia wote wa kima cha juu wasio prosimians au sokwe ni nyani. Kuna takribani spishi 264 wanaofahamika wa kima wanaowakilisha kundikubwa la mamalia wa hali ya juu. Kima huonwa kama ni mwenye akili sana na tofauti na sokwe; kima daima huwa na mikia. Kima wa Dunia ya Kale wanafanana zaidi na sokwe kuliko kima wa Dunia Mpya.
Yaliyomo |
[hariri] Asili
Kutokana na kamusi ya kiingereza ya Oxfoid neno la kimombo ‘monkey’ lenye maana ya kima lilitokana na simulizi za kijerumani ya Reynard the Fox ya mwaka 1580. Katika simulizi hiyo mhusika aliyeitwa Moneke alikuwa ni mtoto wa Martin aliyekuwa sokwe. Neno Moneke laweza kuwa linaweza kuwa linatokana na lugha ya Kitaliano ‘monna’ lenye maana ya sokwe jike. Neno Moneke limedumu sana kutokana na umaarufu wa ‘Reynard The Fox’.
[hariri] Tabia
Kima wanaukubwa tofauti kutoka milimita za urefu 140 – 160 (pamoja na mkia) na uzito wa gramu 120 mpaka 140, mpaka urefu wa mita moja wa kilo 35. Wachache huishi kwenye miti wakati wengine huishi kwenye savana. Chakula chao ni matunda, majani, mbegu, maua, mayai na wanyama wadogo (ikijumuishwa wadudu na buibui). Kima wote wa dunia mpya wana mikia tofauti na wa dunia ya kale. Baadhi ya kima wana uoni wa rangi na wengine hawana. Huku kima wa dunia mpya wakiwa na macho kwa mbele walionekana tofauti hata baina yao hasa pua, mashavu na sehemu ya nyuma kwa ujumla.
[hariri] Uanishaji
Ifuatayo ni orodha ikionesha familia za kima.
- ODA PRIMATES
- Nusuoda Strepsirrhini: komba, koni na lemuri
- Nusuoda Haplorrhini
- Oda ya chini Tarsiiformes
- Familia Tarsiidae: komba vidole-virefu
- Oda ya chini Simiiformes: kima
- Oda ndogo Platyrrhini: kima wa dunia mpya
- Familia Cebidae
- Familia Aotidae
- Familia Pitheciidae
- Familia Atelidae
- Oda ndogo Catarrhini: kima wa dunia ya kale
- Familia ya juu Cercopithecoidea
- Familia ya juu Hominoidea
- Familia Hylobatidae: masokwe wadogo
- Familia Hominidae: masokwe wakubwa na binadamu
- Oda ndogo Platyrrhini: kima wa dunia mpya
- Oda ya chini Tarsiiformes
[hariri] Mahusiano na binadamu
Spishi tofauti za kima wanamahusiano na binadamu baadhi yao hufugwa kama wanyama wa nyumbani na hutumika kama kifani cha binadamu kwenye maabara na safari ya angani. Pia huwahudumia binadamu wenye udhaifu. Kuna baadhi ya maneno kama huonekana kama wanyama waharibifu wa mazao [1] Kima ambao pia wapo kwenye mbuga ya watalii lakini hugeuka kama kitishio kwa watalii huona kama kuna kikwazo kwa binadamu hivyo tatizo dogo. Kwenye dini huwakilisha warevu.
[hariri] Kama huduma kwa watu wasiojiweza
Baadhi ya mashirika yamekuwa wakiwafunza kima wa wakapuchini kama wasaidizi kuwasaidia watu wenye matatizo ya uti wa mgongo na matatizo mengine ya kutembea. Baada ya mafunzo kutosha kima hawa huweza kuwahudumia barabara walemavu wakiwa ndani ya nyumba, kima husaidia kupika kuosha uso na kufungua chupa za vinywaji.
[hariri] Kwenye tafiti
Kima aina ya Macaques wale wa Afrika Green Monkeys, hutumika kwenye tafiti nyingi aidha kwa kukamatwa porini au kulazimiswa. Hutumika sana kutokana na uwezo wao mkubwa wa kubeba vitu, kuzaliana kwa muda mfupi na kufanana kwao sana kisaikolojia na kimaumbile na binadamu.
[hariri] Angani
Nchi nyingi zinawatumia kima kama sehemu yao ya tafiti za anga kujumuisha marekani na Ufaransa. Kima wa kwanza kwenda angani aliitwa Albert IIi, ambaye aliruka angani na roketi ya marekani, mnamo june 14,1949.
[hariri] Kama chakula
Ubongo wa kima unaliwa kama chakula kitamu huko Asia ya kusini, China na Afrika [2]. Kwa taratibu ya dini ya kiislamu kula nyani ni marufuku kabisa. Hata hivyo kima huliwa sehemu nyingine ya Afrika, ambako nyama yake huuzwa kama nyama ya msituni”