Guinea ya Ikweta

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Guinea ya Ikweta (Kiswahili)
Bendera ya Guinea ya Ikweta Nembo ya Guinea ya Ikweta
(Bendera ya Guinea ya Ikweta) (Nembo ya Guinea ya Ikweta)
Lugha rasmi Kihispania, Kifaransa na Kireno
Mji Mkuu Malabo
Mji Mkubwa Bata
Serikali Jamhuri
Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo
Eneo km² 28,050
Idadi ya wakazi 1,308,975 (2018)
Wakazi kwa km² 47
Uchumi nominal Bilioni $12.4
Uchumi kwa kipimo cha umma $9,141
Pesa CFA frank (XFA) (Frank ya Afrika ya Kati)
Kaulimbiu "Uungano, Kazi, Haki"
Wimbo wa Taifa Caminemos pisando las sendas de nuestra inmensa felicidad
(Tuchague njia ya furaha)
Guinea ya Ikweta katika Afrika
Saa za Eneo UTC +1
Mtandao .gq
Kodi ya Simu +240

Jamhuri ya Guinea ya Ikweta (kwa Kiswahili pia: Ginekweta) ni nchi mojawapo ndogo ya Afrika iliyopo upande wa magharibi wa Afrika ya Kati.

Imepakana na Kamerun upande wa kaskazini, Gabon upande wa kusini na mashariki, na Ghuba ya Guinea upande wa magharibi, ambapo visiwa vya São Tomé na Príncipe vinapatikana kusini-magharibi mwa Guinea ya Ikweta.

Jina[hariri | hariri chanzo]

Jina la nchi linatokana na kuwa karibu na Ghuba ya Guinea na Ikweta.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Nchi ina sehemu mbili kuu. Eneo kubwa liko kwenye bara la Afrika katika kanda ya Rio Muni. Ndipo walipo wakazi wengi zaidi.

Sehemu iliyoendelea zaidi, pamoja na mji mkuu, iko kwenye kisiwa cha Bioko. Pamoja na visiwa vingine, hasa Annobon, hiyo kanda ya Visiwa ni sehemu ya pili ya nchi.

Bioko inavyoonekana kutoka Kamerun.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Ilikuwa koloni la Hispania kwa jina la Guinea ya Kihispania likiwa na maeneo mawili ambayo yalijulikana kama Río Muni (bara na visiwa vidogo kadhaa), na kisiwa cha Bioko (zamani: Fernando Poo) ambako uko mji mkuu, Malabo (ambayo iliitwa awali Santa Isabela).

Siasa[hariri | hariri chanzo]

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Mikoa[hariri | hariri chanzo]

Mikoa ya Guinea ya Ikweta

Guinea ya Ikweta imegawiwa katika mikoa 8 iliyopo katika kanda mbili:

  1. Mkoa wa Annobón (mji mkuu wa mkoa: San Antonio de Palé)
  2. Mkoa wa Bioko Norte (Malabo)
  3. Mkoa wa Bioko Sur (Luba)
  4. Mkoa wa Centro Sur (Evinayong)
  5. Mkoa wa Kié-Ntem (Ebebiyín)
  6. mkoa wa Litoral (Bata)
  7. Mkoa wa Wele-Nzas (Mongomo)
  8. Mkoa wa Djibloho (Ciudad de la Paz)

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wananchi wengi (80%) ni wa kabila la Wafang, ambao ni wa Kibantu.

Lugha[hariri | hariri chanzo]

Ni nchi pekee ya Afrika ambapo lugha ya Kihispania ndiyo lugha rasmi na ya taifa, hasa ukiacha Ceuta na Melilla (maeneo ya Hispania yaliyozungukwa na Moroko) na Jamhuri ya Sahara ya Kidemokrasia ya Kiarabu (nchi isiyotambulika kimataifa). Pamoja nacho, Kifaransa na Kireno pia ni lugha rasmi.

Dini[hariri | hariri chanzo]

Wananchi wengi wanafuata Ukristo katika Kanisa Katoliki (88%) na madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (5%). Wanaofuata dini asilia za Kiafrika na Baha'i ni 5%. Waislamu ni 2%.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons

Habari[hariri | hariri chanzo]

Uchambuzi na Maelekezo[hariri | hariri chanzo]

Koo na Makabila[hariri | hariri chanzo]

  • African Pygmies (Utamaduni na mziki wa watu wa Guinea ya ikwete / picha na ukoo.)

Utalii[hariri | hariri chanzo]

Uchumi[hariri | hariri chanzo]


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guinea ya Ikweta kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.