Lesotho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ufalme wa Lesotho
Muso oa Lesotho
Bendera ya Lesotho Nembo ya Lesotho
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Khotso, Pula, Nala
(kwa Kisotho: Amani, Mvua, Ustawi)
Wimbo wa taifa: Lesotho Fatse La Bontata Rona: Lesotho, nchi ya babu zangu
Lokeshen ya Lesotho
Mji mkuu Maseru
29°18′ S 27°28′ E
Mji mkubwa nchini Maseru
Lugha rasmi Kisotho, Kiingereza
Serikali
Letsie III
Moeketsi Majoro
Independence
kutoka Wiingereza
4 Oktoba 1966
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
30,355 km² (140th)
Negligible
Idadi ya watu
 - Julai 2009 kadirio
 - 2004 sensa
 - Msongamano wa watu
 
2,067,000 1 (144)
2,031,348
68.1/km² (138)
Fedha Maloti (LSL)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+2)
(UTC)
Intaneti TLD .ls
Kodi ya simu +266

-


Malealea, mandhari ya Lesotho

Ufalme wa Lesotho, au Lesotho, ni nchi ndogo inayozungukwa na Afrika Kusini pande zote. Haina pwani kwenye bahari yoyote.

Jina Lesotho lamaanisha eneo la Basotho (wakazi 99.7%), watu ambao wanaongea lugha ya Kisotho, ambayo ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza. Wakati wa ukoloni ilijulikana kama Basutoland.

Sasa ni nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa.

Ina wakazi milioni 2 hivi.

Mji mkuu ni Maseru.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Theluji kwenye barabara ya Lesotho

Ukweli wa kijiografia ambao wajulikana zaidi kuhusu Lesotho ni kwamba ni nchi inayozungukwa na Afrika ya Kusini, na ni nchi huru pekee duniani ambayo yote iko juu ya mita 1,000 juu ya usawa wa bahari (UB) (ft 3,281). Eneo la chini zaidi liko mita 1,400 (futi 4,593), na zaidi ya asilimia 80 za nchi ziko juu ya mita 1,800 (futi 5,906).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.

Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.

Lesotho ya sasa ilianza kupatikana mwaka 1822 chini ya chifu Moshoeshoe I aliyeungana na makabila mengine dhidi ya Shaka Zulu (1818-1828).

Baadaye nchi iliathiriwa na mahusiano na Waingereza na Makaburu wa . Koloni la Rasi (leo Afrika Kusini), yakiwemo mapigano ya mara kwa mara.

Wamisionari walioalikwa na Mfalme Moshoeshoe I walianza kuandika na kuchapa kwa lugha ya Kisotho kati ya miaka 1837 na 1855.

Mwaka 1867 nchi ikawa chini ya malkia wa Uingereza kwa jina la Basutoland lakini mwaka 1869, Waingereza waliwaachia Makaburu nusu ya eneo la Basutoland.

Uhuru ulipatikana tena mwaka 1966, na nchi ikaitwa ufalme wa Lesotho.

Siasa[hariri | hariri chanzo]

Makala kuu: Siasa ya Lesotho

Wilaya[hariri | hariri chanzo]

Wilaya.
Makala kuu: Wilaya za Lesotho

Kwa usimamizi wa serikali, Lesotho imegawiwa katika wilaya 10, kila moja ikiongozwa na Karani wa wilaya.

Kila wilaya ina mji unaoitwa mji wa kambi (camptown).

Watu na koo[hariri | hariri chanzo]

Makala kuu: Watu wa Lesotho
Nyumba nchini Lesotho

Wakazi kwa asilimia 90 ni Wakristo, wakigawanyika karibu sawa kati ya Wakatoliki na Waprotestanti wa madhehebu mbalimbali.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Mto Makhaleng, mabonde kwa milima ya Lesotho
Malealea, magharibi mwa Lesotho
Bonde nchini Lesotho

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Makala kuu: Uchumi wa Lesotho


Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Serikali[hariri | hariri chanzo]

Habari[hariri | hariri chanzo]

Uchambuzi[hariri | hariri chanzo]


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Lesotho kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.