Bikira Maria wa Mlima Karmeli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bibi Yetu wa Mlima Karmeli, mchoro wa Pietro Novelli, 1641.

Bikira Maria wa Mlima Karmeli ni jina linalopewa Bikira Maria kama msimamizi wa Wakarmeli. Wa kwanza wao walikuwa wakaapweke walioishi mwishoni mwa karne ya 12 na mwanzoni mwa karne ya 13 katika Nchi Takatifu juu ya Mlima Karmeli, ambapo zamani Nabii Eliya alirudisha Waisraeli kumuabudu Mungu aliye hai.

Katikati ya makazi yao walijenga kikanisa kwa heshima ya Bikira Maria, msimamizi wao.

Tangu karne ya 15 watu wamemheshimu kwa jina hilo hasa kwa kuvaa skapulari ya kahawia inayosemekana Maria alimpa Mkarmeli Simoni Stock (1165-1265).

Kumbukumbu katika liturujia inafanyika tarehe 16 Julai.[1][2][3][2]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Martyrologium Romanum
  2. 2.0 2.1 Bede Edwards, OCDS. "St. Simon Stock—The Scapular Vision & the Brown Scapular Devotion." Carmel Clarion Volume XXI, pp 17–22, July–August 2005, Discalced Carmelite Secular Order, Washington Province.
  3. Scapular Devotion." July–August 2005, Discalced Carmelite Secular Order, Washington Province.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bikira Maria wa Mlima Karmeli kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.