Shirikisho la Mikronesia
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: | |||||
Wimbo wa taifa: Patriots of Micronesia | |||||
![]() | |||||
Mji mkuu | Palikir | ||||
Mji mkubwa nchini | Weno | ||||
Lugha rasmi | Kiingereza (kitaifa), Kiulithi, Kiwoleaia, Kiyap, Kipohnpeia, Kikosraea, and Kichuuk (kijimbo) | ||||
Serikali | Jamhuri Peter M. Christian | ||||
Uhuru Tarehe |
3 Novemba 1986 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
702 km² (ya 188) | ||||
Idadi ya watu - Julai 2006 kadirio - 2000 sensa - Msongamano wa watu |
106,104 (ya 192) 107,000 158.1/km² (ya 75) | ||||
Fedha | US Dollar (USD )
| ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC+10) (UTC-) | ||||
Intaneti TLD | .fm | ||||
Kodi ya simu | +691
- |
Shirikisho la Mikronesia ni nchi ya visiwani katika Pasifiki kaskazini kwa Papua Guinea Mpya.
Ni nchi huru inayoshirikiana na Marekani. Nchi ilikuwa eneo lindwa chini ya Marekani kwa niaba ya Umoja wa Mataifa hadi ikapata uhuru wake mwaka 1986.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Shirikisho lajumlisha sehemu kubwa ya funguvisiwa la Karolini katika Mikronesia, kanda la Pasifiki. Jumla ya visiwa ni 607.
Nchi ina majimbo manne ya kujitawala ambayo ni Chuuk, Kosrae, Pohnpei na Yap.
Visiwa vya Palau ni pia sehemu ya Karolini lakini ni nchi ya pekee.
Mji mkubwa wa nchi ni Weno (wakazi 17,624) kisiwani Chuuk lakini mji mkuu ni Palikir kwenye kisiwa cha Pohnpei.
Majimbo ya shirikisho[hariri | hariri chanzo]
Kuna majimbo manne kama yafuatayo:
Bendera | Jimbo | Mji Mkuu | Eneo la nchi kavu[1] | Wakazi[2] | Msongamano |
---|---|---|---|---|---|
![]() |
Chuuk | Weno | 127 km2 | 53,595 | 1,088 per km2 |
![]() |
Kosrae | Tofol | 110 km2 | 7,686 | 70 per km2 |
Pohnpei | Palikir | 346 km2 | 34,486 | 100 per km2 | |
![]() |
Yap | Colonia | 118 km2 | 11,241 | 95 per km2 |
Historia[hariri | hariri chanzo]
Visiwa vimekaliwa na watu tangu miaka 4,000 iliyopita, hasa kutoka Rasi ya Malay na visiwa vya Indonesia. Wengine wametokea visiwa vya Polinesia.
Kisiwani Yap kulitokea dola na utawala wa kifalme.
Tangu kufika kwa Wahispania katika karne ya 16 visiwa vilikuwa chini ya ubwana wa nje lakini maisha ya kawaida yaliendelea bila mabadiliko makubwa kwa muda mrefu.
Mwisho wa karne ya 19 Hispania iliuza koloni kwa Ujerumani; utawala wa Kijerumani ulikwisha katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ukachukuliwa na Japani hadi mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Japani ilifuatwa na Marekani iliyoendelea kutawala kwa niaba ya UM hadi uhuru.
Lugha na utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Kuna lugha 18 ambazo huzungumzwa katika Shirikisho la Mikronesia.
Wakazi wengi ni wa makabila ya asili.
Upande wa dini, wengi ni Wakristo, kwanza Wakatoliki halafu Waprotestanti wa madhehebu mbalimbali.
Uchumi[hariri | hariri chanzo]
Uchumi wa nchi hutegemea hasa kilimo cha kujisukuma na uvuvi. Mapato ya serikali ni kutokana na vibali kwa wavuwi wa nje wanaovua samaki ndani ya maji ya shirikisho.
Kuna pia uchimbaji wa fosfeti.
Hata hivyo shirikisho la Mikronesia pamoja na Nauru vina idadi kubwa ya watu wanene duniani.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
Nchi_na maeneo ya Australia na Pasifiki |
Australia | Fiji | Guam | Hawaii | Kaledonia Mpya | Kiribati | Kisiwa cha Pasaka | Mikronesia | Nauru | Nyuzilandi | Niue | Pitcairn | Polynesia ya Kifaransa | Palau | Papua Guinea Mpya | Samoa | Samoa ya Marekani | Visiwa vya Cook | Visiwa vya Mariana ya Kaskazini | Visiwa vya Marshall | Visiwa vya Solomon | Tonga | Tuvalu | Vanuatu | Wallis na Futuna |
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|