Songwe (Mbeya)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mto Songwe)
Mto Songwe (juu kushoto)

Songwe ni jina la mito miwili ya Tanzania: mmoja uko katika mkoa wa Mbeya, mwingine katika mkoa wa Songwe.

Songwe ya Kusini ina chanzo chake katika milima ya Umalila karibu na Santilya ikielekea kusini na kuishia Ziwa Nyasa. Baada ya kupita Itumba (Ileje) mto ni mpaka kati ya Tanzania na Malawi.

Tabia yake ya kubadilisha-badilisha mwendo wake imesababisha matatizo kati ya nchi jirani kwa sababu mashamba ya watu yamepatikana mara upande mmoja mara upande mwingine wa mpaka wa kimataifa.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]