Historia ya Uswisi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Historia ya Uswisi inahusu eneo ambalo siku hizi linaunda Jamhuri ya Uswisi.

Shirikisho la Uswisi lilianza mwaka 1300 hivi kutokana na ushindi vitani dhidi ya Austria na Burgundy.

Uhuru wa shirikisho kutoka Dola Takatifu la Kiroma ulitambuliwa rasmi katika Amani ya Westphalia mwaka 1648.

Uswisi imepata umaarufu hasa kutokana na nchi kutoshiriki katika vita kwa zaidi ya miaka 300 ambapo watu wenye utamaduni tofauti na nchi jirani wameshirikiana karne nyingi kwa amani.

Ni nchi iliyotunza demokrasia tangu karne nyingi bila kuwa na vipindi vya udikteta au utawala wa mabavu, tena demokrasia ya moja kwa moja ambako wananchi wa kawaida wana haki ya kutunga au kubadilisha sheria kwa njia ya kura ya maoni ya watu wote.

Hali hiyo imechangia kuifanya nchi yenye benki zenye sifa kote duniani.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Uswisi kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.