Historia ya Ugiriki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Historia ya Ugiriki inahusu eneo ambalo siku hizi linaunda Jamhuri ya Ugiriki.

Ugiriki ni nchi yenye historia ndefu na maarufu sana, hata inaitwa "nchi mama ya Ulaya".

Ugiriki wa Kale[hariri | hariri chanzo]

Ugiriki ya Kale ni kipindi cha historia ambapo Ugiriki ulipanuka katika eneo kubwa la Mediteranea na Bahari Nyeusi, na kudumu kwa karibu milenia moja, hadi Ukristo ulipoanza.

Unadhaniwa na wanahistoria wengi kuwa ni utamaduni anzilishi wa ustaarabu wa magharibi. Utamaduni wa Kigiriki ulikuwa na nguvu kubwa ya ushawishi katika Dola la Roma, ambalo lilibeba sehemu ya utamaduni huo katika sehemu nyingi za Ulaya.

Ustaarabu wa Ugiriki ya kale umeathiri pia lugha, siasa, mifumo ya elimu, falsafa, sayansi, sanaa, ufundi sanifu wa dunia ya kisasa, na kuchochea Mwamko Mpya katika Ulaya Magharibi.

Halafu ukachipuka tena katika vipindi mbalimbali vya uamsho wa tamaduni za kisasa za Kigiriki, ndani ya karne ya 18 na ya 19 katika Ulaya na Amerika.

Ugiriki wa sasa[hariri | hariri chanzo]

Ugiriki ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 1981.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Ugiriki kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.