Historia ya Polandi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Polandi chini ya Mieszko I, mwanzilishi wa taifa (960–992).
Shirikisho la Warsaw katika kilele cha uenezi wake (1635).

Historia ya Polandi inahusu eneo ambalo leo linaunda Jamhuri ya Polandi.

Waslavi walienea kati nchi katika nusu ya pili ya karne ya 5 BK.

Ukristo wa Kikatoliki kupokewa na mfalme Mieszko I (960-992) na Wapolandi kwa jumla (966) hutazamiwa kama chanzo cha taifa lao la pekee katika jamii ya Waslavi.

Nchi ilistawi na kuenea hasa chini ya ukoo wa Wajageloni (13861572).

Katika miaka ya 15691795 Polandi iliunganishwa na Lithuania katika shirikisho la kifalme. Mfalme wa Polandi alikuwa pia mtawala wa Lithuania, na tangu mapatano ya Lublin nchi hizo mbili zilikuwa na bunge la pamoja, lakini kila sehemu iliendelea na sheria zake na jeshi la pekee. Bunge la pamoja lililokuwa hasa mkutano wa makabaila wote lilikuwa na mamlaka ya kumchagua mfalme likapata ushawishi mkubwa.

Wagombea wa ufalme waliachana na mamlaka za kifalme wakijaribu kupata kura nyingi za wabunge na hivyo nguvu ya dola ilififia.

Mwaka 1764 nchi ilianza kurudi nyuma na zile za jirani, yaani Urusi, Austria na Prussia, ziligawana kwa awamu tatu (1772, 1793, 1795) eneo lake lote. Yaani kuanzia mwaka 1772 majirani hayo matatu ya Polandi yalivamia shirikisho na kugawana maeneo yake. Kufikia mwaka 1795 maeneo yote yalikwisha kugawiwa kati ya majirani hao.

Wapolandi walijaribu mara kadhaa kujikomboa, lakini walipata uhuru kwa muda tu (1807-1815 na 1918-1939).

Wapolandi walijaribu mara kadha kujikomboa, lakini walipata uhuru kwa muda tu (1807-1815 na 1918-1939).

Baada ya vita vikuu vya pili, Polandi ikawa chini ya utawala wa Kikomunisti hadi ilipofaulu kujikomboa (1989).

Poland imekuwa nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu tarehe 1 Mei 2004.

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Polandi kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.