Waarabu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mwarabu)
Waarabu duniani
     Jumuiya ya Kiarabu      + 5,000,000      + 1,000,000      + 100,000

Waarabu (kwa Kiarabu عَرَبِ, matamshi ya Kiarabu: [ʕarabi]) ni watu ambao lugha mama yao ni Kiarabu wakijitambua vile.

Asili ya Waarabu na uenezaji[hariri | hariri chanzo]

Kiasili walikuwa watu wa Bara Arabu na maeneo jirani katika Syria na Iraki[1], lakini tangu kuja kwa Uislamu walienea nje ya eneo asilia hasa katika Afrika ya Kaskazini na nchi za Mashariki ya Kati ambako walijichangaya na wenyeji ambao wengi wao wamepokea lugha ya Kiarabu tangu karne nyingi na kujitazama kama Waarabu pia.

Kutokana na uhamiaji wako pia katika Afrika ya Mashariki, Visiwa vya Komoro na visiwa vingine vya Bahari Hindi, Amerika, Ulaya Magharibi, Indonesia, Uhindi na Iran. [2] [3] [4] [5] [6]

Dini ya Uislamu ilianzia kati ya Waarabu na hivyo Kiarabu ndiyo lugha ya Qurani na maandiko ya Kiislamu, na Waarabu wengi ni Waislamu. Walakini kati ya Waislamu wote Waarabu ni kama asilimia 20 tu. [7]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kihistoria Waarabu walitajwa mara ya kwanza wakati wa karne ya 9 KK kama makabila ya mashariki na kusini mwa Syria na kaskazini mwa Bara Arabu. [8] Waarabu wanaonekana walikuwa chini ya wafalme wa Milki ya Ashuru (911-612 KK), na baadaye chini ya Milki ya Babeli iliyofuata (626-539 KK), Waakhemi (539-332 KK), Waseleukidi na Waparthi.

Katika karne ya 3 KK Waarabu wa Nabatea waliunda ufalme wao karibu na Petra katika Yordani ya leo. Makabila ya Kiarabu kama Waghassanidi na Walakhmidi huanza kuonekana katika jangwa la Syria Kusini kuanzia katikati ya karne ya 3 BK wakiunda milki zao zilizoshirikiana na Dola la Roma na Wasasani. Hadi karne ya 7 sehemu ya Waarabu hasa wa magharibi mwa eneo lao walikuwa Wakristo, wengine pia Wayahudi.

Baada ya Muhamad, makhalifa wa kwanza (632-661 BK) waliunganisha Waarabu wote chini ya utawala wao wakaendelea kuvamia milki jirani za Dola la Roma na Uajemi ya Wasasani. ote walianza kutumia lugha ya Kiarabu kama lugha ya utawala. Makabila mengi kutoka Bara Arabu yalianza kuhamia nchi zilizovamiwa katika hiyo milki kubwa ya Kiislamu iliyoenea kutoka Moroko na Hispania upande wa magharibi hadi mipaka ya China na Uhindi upande wa mashariki.[9] Katika karne zilofuata, wakazi wengi wa maeneo hayo walianza kuwa Waislamu na kutumia Kiarabu kama lugha ya kidini na ya kielimu; hasa katika sehemu kubwa ya Afrika Kaskazini pamoja na Misri na katika nchi za Asia Magharibi (hasa nchi za leo Syria, Lebanoni, Iraki) wenyeji wengi walianza kutumia Kiarabu kama lugha yao na hivyo kuitwa Waarabu.

Kwa karne nyingi Waarabu hao walitawaliwa na Milki ya Osmani[10]. Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914-1918) milki hiyo ilivunjwa na kugawiwa kwa maeneo ya nchi za Kiarabu za leo[11] ambazo kwa muda mfupi zilitawaliwa bado kama makoloni au nchi lindwa chini ya Uingereza na Ufaransa.

Mwaka 1945 nchi hizo ziliunda Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.[12]

Wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.

Nchi za Waarabu[hariri | hariri chanzo]

Leo hii Waarabu kimsingi hukalia nchi 22 wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu. Nchi hizo zinaenea kwa kilomita za mraba milioni 13 kutoka bahari ya Atlantiki upande wa magharibi hadi Bahari ya Kiarabu katika mashariki na kutoka Bahari ya Mediterranean katika kaskazini hadi Pembe ya Afrika na Bahari ya Hindi katika kusini. Watu wasio Waarabu wakitumia lugha zao za pekee huishi pia katika nchi hizo, wakati mwingine wakiwa wengi. Hawa ni pamoja na Wasomali, Wakurdi, Waberberi, Waafar, Wanubi na wengineo .

Uenezaji wa lugha[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa kuzaliwa kwa Mtume Muhamad lugha ya Kiarabu ilitumika Uarabuni tu, nchi ya jangwa na oasisi. Kutoka hapa makabila ya Waarabu Waislamu walivamia nchi jirani ambako wenyeji walitumia lugha mbalimbali. Lugha kadhaa zimeendelea kwa viwango vidogo, vingine vimebaki na nguvu zaidi. Lugha ya Kiaramu iliyowahi kutamalaki katika siasa na uchumi kuanzia Syria hadi Uajemi na zaidi, imebaki kati watu wa vijiji katika maeneo ya kaskazini ya Syria na Iraki, pia kama lugha ya liturgia kanisani. Kikopti iliyokuwa lugha ya Misri imebaki pekee katika liturgia ya kanisa ilhali Wakristo Wakopti wanaongea Kiarabu tu. Kiberber bado inazungumzwa na milioni kadhaa katika Moroko na Algeria. Kikurdi ina nguvu katika milima ya Syria na Iraki kaskazini. Kiajemi (lugha ya Iran) kimefaulu kurudi kama lugha ya kitaifa lakini imepokea karibu asilimia 40 za msamiati wake kutoka Kiarabu; atahri kubwa ya lugha ya Kiarabu inaonekana pia katika lugha nyingine nyingi hadi Kiswahili.

Katika nchi zinazoitwa Kiarabu, lugha ya Kiarabu imekuwa lugha ya kila siku ya kuongea na pia ya serikali, biashara na utamaduni hata kwa hao ambao bado wmetunza lugha nyingine kama lugha yao ya kwanza[13].

Dini[hariri | hariri chanzo]

Kwa upande wa dini, Waarabu huwa na tofauti kati yao.

Katika zama za kabla ya Uislamu, Waarabu wengi walifuata dini za kuabudu miungu mingi. Makabila kadhaa yalikuwa yamekubali Ukristo au Uyahudi na watu wachache waliotwa hanif walisemekana kuwa na imani kwa Mungu mmoja. [14]

Leo, karibu asilimia 93 za Waarabu ni wafuasi wa Uislamu [15]. Kuna pia Wakristo kama jumuiya ndogo zaidi. [16] Waislamu Waarabu kimsingi ni wa madhehebu ya Wasunni, Washiia, Waibadi na Waalawi.

Wakristo wa Kiarabu kwa ujumla hufuata moja ya Makanisa ya Kikristo ya Mashariki, kama yale yaliyo ndani ya makanisa ya Orthodox ya Mashariki, makanisa Katoliki ya Mashariki, au makanisa ya Kiprotestanti ya Mashariki. [17] Kuna pia idadi ndogo ya Wayahudi wa Kiarabu ambao bado wanaishi katika nchi za Kiarabu lakini wengi wao waliondoka kwao wakihamia Israeli au nchi nyingine za Ulaya na Amerika. Sehemu ya Wakristo katika nchi za Kiarabu hawajitambui kuwa Waarabu kwa mfano Wakopti au Waashuri.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Mabry, Tristan James (2015). Nationalism, Language, and Muslim Exceptionalism. University of Pennsylvania. pp. 53–85. ISBN 9780812246919. Retrieved 23 May 2021. 
  2. Frishkopf, Michael, ed. (2010). Music and media in the Arab world (1st ed.). Cairo: The American University in Cairo Press. ISBN 978-977-416-293-0. 
  3. Bureš, Jaroslav (2008). Main characteristic and development trends of migration in the Arab world. Prague: Institute of International Relations. ISBN 978-80-86506-71-5. 
  4. Arab (People). Britannica. Iliwekwa mnamo 19 December 2020.
  5. Bureš, Jaroslav (2008). Main characteristic and development trends of migration in the Arab world. Prague: Institute of International Relations. ISBN 978-8086506715. 
  6. Chapter 4. Modern Standard Arabs". Nationalism, Language, and Muslim Exceptionalism, Philadelphia: University of Pennsylvania Press, 2015, pp. 53-85. https://doi.org/10.9783/9780812291018.53
  7. Demographics of Islam. Jalada kutoka ya awali juu ya 9 October 2020. Iliwekwa mnamo 28 September 2020.
  8. Myers, E. A. (11 February 2010). The Ituraeans and the Roman Near East: Reassessing the Sources. Cambridge University Press. p. 18. ISBN 978-1-139-48481-7. 
  9. Ruthven, Albert Hourani; with a new afterword by Malise (2010). A history of the Arab peoples (1st Harvard Press pbk. ed.). Cambridge, Mass.: Belknap Press of Harvard University Press. ISBN 978-0-674-05819-4. 
  10. "The Arab Revolt, 1916-18 | The Ottoman Empire." New Zealand History. Ministry for Culture and Heritage. 30 July 2014.
  11. Rogan, Eugene L. (2004). Frontiers of the state in the late Ottoman Empire : Transjordan, 1850–1921. Cambridge University Press. ISBN 978-0-521-89223-0. OCLC 826413749. 
  12. "Arab League formed | This Day in History — 3/22/1945." HISTORY. US: A&E Television Networks. 2010. Retrieved on 28 April 2014.
  13. Bernard Ellis Lewis; Buntzie Ellis Churchill (2008). Islam: The Religion and the People. Pearson Prentice Hall. p. 137. Retrieved 21 August 2017. At the time of the Prophet's birth and mission, the Arabic language was more or less confined to Arabia, a land of deserts, sprinkled with oases. Surrounding it on land on every side were the two rival empires of Persia and Byzantium. The countries of what now make up the Arab world were divided between the two of them—Iraq under Persian rule, Syria, Palestine, and North Africa part of the Byzantine Empire. They spoke a variety of different languages and were for the most part Christians, with some Jewish minorities. Their Arabization and Islamization took place with the vast expansion of Islam in the decades and centuries following the death of the Prophet in 632 CE. The Aramaic language, once dominant in the Fertile Crescent, survives in only a few remote villages and in the rituals of the Eastern churches. Coptic, the language of Christian Egypt before the Arab conquest, has been entirely replaced by Arabic except in the church liturgy. Some earlier languages have survived, notably Kurdish in Southwest Asia and Berber in North Africa, but Arabic, in one form or another, has in effect become the language of everyday speech as well as of government, commerce and culture in what has come to be known as "the Arab world." 
  14. Berkey, Jonathan Porter (2003). The Formation of Islam: Religion and Society in the Near East, 600–1800. Cambridge University Press. p. 42. ISBN 978-0-521-58813-3.  Unknown parameter |url-access= ignored (help)
  15. Arabs facts, information, pictures. Encyclopedia.com articles about Arabs (21 April 2018). Iliwekwa mnamo 9 May 2018.
  16. Religious Diversity Around The World – Pew Research Center. Pew Research Center's Religion & Public Life Project (4 April 2014).
  17. Phares (2001). Arab Christians: An Introduction. Arabic Bible Outreach Ministry.