Jimbo katoliki la Tanga
Mandhari
(Elekezwa kutoka Jimbo Katoliki la Tanga)
Jimbo Katoliki la Tanga (kwa Kilatini "Dioecesis Tangaënsis") ni mojawapo kati ya majimbo 36 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania na kama hayo yote linafuata mapokeo ya Roma.
Makao makuu yake yako katika mji wa Tanga na linahusiana na Jimbo Kuu la Dar-es-Salaam.
Askofu wa jimbo ni Thomas John Kiangio.
Historia
[hariri | hariri chanzo]- 18 Aprili 1950: Kuanzishwa kama Apostolic Prefecture ya Tanga kutokana na Apostolic Vicariate ya Kilimanjaro
- 24 Februari 1958: Kufanywa jimbo kamili.
Uongozi
[hariri | hariri chanzo]- Maaskofu wa Tanga
- Thomas John Kiangio (7 Juni 2023 - )
- Anthony Banzi (10 Juni 1994 - 20 Desemba 2020)
- Telesphore Mkude (18 Januari 1988 – 5 Aprili 1993)
- Maurus Gervase Komba (15 Desemba 1969 – 18 Januari 1988)
- Eugène Cornelius Arthurs, I.C. (24 Februari 1958 – 15 Desemba 1969)
- Prefect Apostolic wa Tanga
- Askofu Eugène Cornelius Arthurs, I.C. (9 Juni 1950 – 24 Februari 1958)
Takwimu
[hariri | hariri chanzo]Eneo la jimbo ni km2 26,807, ambapo kati ya wakazi 1,650,000 (2004) kulikuwa na Wakatoliki 180,000 (10.9%).
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]| Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Jimbo katoliki la Tanga kama historia yake au maelezo zaidi? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |