Dola la Songhai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Eneo la Dola la Songhai

Dola la Songhai ni dola lililostawi Afrika Magharibi hasa katika karne ya 14 hadi karne ya 16.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Asili ya Wasonghai ilikuwa Nigeria ya Kaskazini ya leo. Walipanua utawala wao kuelekea magharibi wakapokea Uislamu wakati wa uvamizi wa Almurabitun.

Mnamo mwaka 1250 walikuwa chini ya milki ya Mali lakini katika karne ya 14 walijipatia uhuru tena, wakaanza kushika maeneo ya Mali yenyewe.

Kilele cha nguvu yake ilikuwa wakati wa mfalme Askia Mohammad I katika karne ya 16 walipotawala eneo kubwa kutoka Kano (Nigeria) hadi pwani ya Atlantiki. Wakati wake mji wa Timbuktu ilitembelewa na msafiri Leo Africanus aliyeleta baadaye habari za nchi hadi Ulaya.

Uchumi wa dola ulisimama kwenye udhibiti wa biashara ya misafara kuvukia Sahara na pia kwenye mto Niger. Biashara iliyotumia njia za bahari ya Atlantiki haikupatikana hadi mnamo mwaka 1400.

Bidhaa zilizosafirishwa zilikuwa hasa dhahabu na chumvi, pamoja na biashara ya watumwa kuvukia Sahara. Njia kuu ya misafara ilivuka Fezzan kupitia Bilma, Agadez na Gao.[1]

Bandari kuu kwenye mto Niger ilkuwa mji wa Timbuktu ambako misafara ilihamisha bidhaa zao kutoka ngamia kwa mashua za mtoni.

Utawala wao uliporomoka baada ya mashambulizi kutoka Moroko mwaka 1591. Wakati ule mataifa ya Ulaya yameshaanza kufika kwenye mwambao wa Afrika ya Magharibi wakifungua biashara ya moja kwa moja na Ulaya. Umuhimu wa biashara ya ng'ambo ya Sahara ulipungua vikali pamoja na faida iliyopatikana kwa watawala katika maeneo ya Sahel.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Willard, Alice (1993-04-01). "Gold, Islam and Camels: The Transformative Effects of Trade and Ideology". Comparative Civilizations Review. 28 (28): 88–89. ISSN 0733-4540

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Dola la Songhai kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.