Wafinisia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Miji muhimu na njia za biashara za Wafinisia

Wafinisia (au Wafoinike) walikuwa wakazi wa Finisia ambao zamani za Nyakati za Kale waliishi kwenye mwambao wa mashariki wa Bahari ya Mediteranea.

Miji-dola yao ilikaa katika eneo la nchi za kisasa za Lebanoni na Syria.

Wafinisia walizungumza Kifinisia kilichokuwa lugha ya Kisemiti ambayo ilipotea baada ya kusambaa kwa Kiarabu tangu karne ya 7.

Walikuwa wafanyabiashara na mabaharia hodari sana. Walijenga utajiri wao juu ya biashara ya ubao kutoka milima ya Lebanoni. Hasa miti ya aina ya seda (Cedrus Libani) ilitafutwa sana.

Baadaye waliunda makoloni yao katika magharibi ya Mediteranea hadi Hispania. Lakini koloni lao mashuhuri lilikuwa Karthago (Afrika ya Kaskazini).

Mafanikio ya kihistoria ya Wafinisia[hariri | hariri chanzo]

Wafinisia (kama si Wakananayo) walianzisha mwandiko wa pekee uliokuwa chanzo cha alfabeti zote za Ulaya kupitia alfabeti ya Kigiriki.

Mabaharia Wafinisia walikuwa watu wa kwanza waliozunguka bara la Afrika kwa jahazi zao. Safari hiyo ilitokea kama mwaka 600 KK kwa niaba ya mfalme Neko II wa Misri aliyewaajiri kwa safari ile.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]