Epifania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mamajusi Balthasari, Melkiori na Gaspari, katika mozaiki ya karne ya 6 ndani ya Basilika la Sant'Apollinare Nuovo mjini Ravenna, Italia.
Mwaka wa Kanisa kadiri ya kalenda ya liturujia ya Roma kama kielelezo cha kawaida kwa Wakristo wa magharibi.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki

Epifania ni neno linatokana na Kigiriki ἐπιφάνεια, epifaneia, yaani udhihirishaji, tokeo, ujio, uwepo wa Mungu.

Kwa kifupi zaidi 'Eπιφάνια (Yohane Krisostomo) linamaanisha "Kuzaliwa kwa Yesu Kristo", kwa kuwa ndivyo Bwana alivyotutokea sisi binadamu kadiri ya imani ya Wakristo.

Kwa kawaida Epifania inaeleweka kama sikukuu muhimu mojawapo ya Ukristo ambayo inahusiana na Noeli na inaadhimishwa kimapokeo tarehe 6 Januari. Lakini, kuanzia mwaka 1970, Kanisa la Kilatini limeruhusu Wakatoliki wa nchi ambapo tarehe hiyo si sikukuu ya taifa, waiadhimishe katika Jumapili ya kwanza baada ya Januari mosi, isije ikasahaulika. Upande wao, Makanisa ya Kiorthodoksi yanayofuata bado Kalenda ya Juliasi wanaiadhimisha siku ambayo katika nchi nyingi ni tarehe 19 Januari, kutokana na tofauti ya siku 13 kati ya kalenda hiyo na ile ya Gregori.

Mbali ya kushiriki ibada kanisani, desturi zinazohusiana na Epifania ni pamoja na nyimbo maalumu, kuandika majina ya mamajusi katika milango kwa chaki, kubariki nyumba, kula keki ya mamajusi watatu, kuogelea na kuondoa mapambo ya Krismasi.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Neno ἐπιφάνεια lilitumiwa na Wagiriki wa kale kumaanisha tendo ambalo mungu mmojawapo aliweza kujidhirisha kwa binadamu (kwa njia ya miujiza, njozi, ishara, n.k.).

Katika karne ya 3 Wakristo walianza kulitumia kuhusu matendo ambayo Yesu alijidhirisha (kama vile miujiza yake, ishara n.k.).

Kwa namna ya pekee, kati ya matendo hayo yalisisitizwa:

Katika adhimisho la Epifania, Wakatoliki wanasisitiza zaidi ujio wa mamajusi, kumbe Waorthodoksi wanasisitiza ubatizo wa Yesu, Utatu Mtakatifu ulipojitokeza: Baba katika sauti kutoka mbinguni, Mwana katika mwili alioutwaa, na Roho Mtakatifu katika umbo la njiwa aliyemshukia Yesu.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Epifania kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.