Mbawakimia kijani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Chrysopidae)
Mbawakimia kijani
Chrysoperla carnea
Chrysoperla carnea
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Neuroptera (Wadudu walio na mabawa wenye vena nyingi kama kimia)
Nusuoda: Hemerobiiformia (Mbawakimia)
Familia ya juu: Chrysopoidea (Mbawakimia kijani)
Familia: Chrysopidae
Schneider, 1851
Ngazi za chini

Nusufamilia 3:

Mbawakimia kijani ni wadudu wadogo kiasi wa familia Chrysopidae katika oda Neuroptera (wadudu mabawa-vena) walio na mabawa yanayofanana na kimia. Kama jina lao linavyoonyesha wana rangi ya kijani kwa kawaida, huku mbawakimia kahawia (familia Hemerobiidae) wakiwa kahawia kwa wazi.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Kichwa kwa karibu cha Apertochrysa edwardsi kutoka Austins Ferry, Tasmania

Mbawakimia kijani ni wadudu dhaifu wenye urefu wa mwili wa mm 8 hadi 40 na upana wa mabawa wa mm 10 hadi zaidi ya 65, wakubwa zaidi wakiwa spishi za kitropiki. Kwa kawaida mwili wao huwa kijani kibichi hadi hudhurungi-kijani, na machomzolenzi yanaonekana kuwa ya dhahabu katika spishi nyingi. Mabawa ni mangavu yenye kugeuzwa-geuzwa.rangi kidogo. Baadhi wana vena kijani za mabawa, wengine ruwaza ya mabawa ya rangi ya hudhurungi. Zinaposhughulikiwa spishi za baadhi ya jenasi, kama vile Chrysopa na Cunctochrysa, hutoa harufu mbaya kutoka kwa jozi ya tezi za prothoraksi.

Wapevu wana viwambosikio kwenye matako ya mabawa vinavyowawezesha kusikia vizuri. Baadhi ya spishi za Chrysopa huonyesha [[tabia] ya kukwepa wanaposikia miito ya kiukasauti ya popo. Wakati wa kuruka hufunga mabawa yao (ili kufanya ishara yao ya mwangwi kuwa ndogo) na kushuka chini. Mbawakimia kijani pia hutumia mitetemo ya uso wa chini au ya mwili kama njia ya mawasiliano kati yao, haswa wakati wa uchumba. Spishi zilizo takriban sawa kimofolojia zinaweza pengine kutengwa kwa urahisi zaidi kulingana na ishara zao za kujamiiana. Kwa mfano, Chrysoperla mediterranea wa Ulaya ya Kusini anaonekana takriban sawa na jamaa yake ya kaskazini C. carnea, lakini "nyimbo" zao za uchumba ni tofauti sana. Wana wa spishi moja hawatajibu mitetemo ya wengine[1].

Wapevu hukiakia wakati wa utusitusi au usiku. Hula mbelewele, mbochi na mana kuongezwa na matitiri, vidukari na arithropodi wengine wadogo. Baadhi, hasa Chrysopa, ni mbuai haswa. Wengine hula mbochi na vitu kama hivyo takriban peke yao, na huwa na hamira zinazoishi pamoja katika njia ya mmeng'enyo ili kusaidia kupasuka-pasuka chakula kuwa virutubishi.[2]

Mayai ya spishi fulani juu ya vikonyo nchini Ujerumani
Lava wa Chrysoperla carnea akijilisha na kidukari

Mayai hutagwa usiku, moja moja au kwa vikundi vidogo. Jike mmoja hutoa mayai 100-200, ambayo huwekwa kwenye mimea, kwa kawaida ambapo vidukari hupatikana karibu kwa tele. Kila yai hutundikwa kwenye kikonyo chembamba chenye urefu wa sm 1, kwa kawaida kwenye upande wa chini wa jani. Mara tu akitoka, lava hubambua, kisha hutambaa juu ya kikonyo cha yai ili kujilisha. Lava wana umbo jembamba zaidi lenye nundu kwenye thoraksi au ni wanene wenye nywele ngumu ndefu zinazotoka kando. Nywele hizi hukusanya uchafu na mabaki ya chakula (kutikulo tupu za vidukari haswa) ambayo hupatia kamafleji kwa ndege.

Lava ni mbuai walafi wanaoshambulia wadudu wengi wa saizi inayofaa, haswa wenye miili myororo kama vile vidukari, viwavi, lava wa wadudu wengine, mayai ya wadudu na, ikiwa wako wengi sana, pia kila mmoja. Lava wanaweza pia kuuma binadamu mara kwa mara, labda kwa sababu ya uchokozi au njaa[3]. Kwa hivyo, lava hujulikana kwa lugha ya kawaida kama "simba wa vidukari" au "mbwa mwitu wa vidukari", sawa na simba-sisimizi wanaohusiana. Hisia zao hazikuendelezwa vizuri, isipokuwa kwamba ni nyeti sana kwa kuguswa. Wakitembea kwa njia ovyo-ovyo lava huzungusha kichwa chao kutoka upande mmoja hadi mwingine na wanapopiga kitu kinachoweza kuwa mbuawa lava hukishika. Maxila zao zina uwazi ndani yao, hivyo kuruhusu uto wa mmeng'enyo kuingizwa ndani ya mbuawa ambao unaweza kuyeyusha ogani za kidukari katika sekunde 90. Kulingana na hali ya mazingira badiliko kuwa bungo, ambalo hufanyika kwenye kifukofuko, huchukua muda wa wiki 1-3. Spishi kutoka maeneo ya halijoto ya wastani hupitia majira ya baridi kama hatua kabla bungo, ingawa C. carnea hupitia kama wapevu waliobambua juzijuzi.

Matumizi katika udhibiti wa kibiolojia wa wasumbufu[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na spishi na hali ya mazingira, baadhi ya mbawakimia kijani watakula tu vitu 150 vya mawindo katika maisha yao yote, huku wengine hula vidukari 100 katika wiki moja. Kwa hivyo, katika nchi kadhaa, mamilioni ya Chrysopidae walafi kama hawa hukuzwa ili kuuzwa kama wadhibiti wa kibiolojia wa wadudu na matitiri wasumbufu katika kilimo na bustani. Wanasafirishwa kama mayai kwa kuwa, kama ilivyoonyeshwa hapo juu, wako wakali sana na hula wenzao katika visanduku. Mayai husambazwa kati ya mimea iliyoathiriwa ambapo hutoka kwenye mayai na lava hufanya kazi yao muhimu. Walakini, utendaji wao ni tofauti tofauti. Kwa hivyo utafiti zaidi unahitajika ili kuboresha ufanisi wa mbawakimia kijani kama mbinu wa udhibiti wa kibiojia wa wadudu wasumbufu. Spishi ambazo hadi sasa zimevutia utafiti mpana na zinapatikana kwa urahisi mzuri kiasi, ni wana kadhaa wa Chrysoperla pamoja na Mallada signatus. Ni mbuai wa asili wa kifukulile wa Ulaya (Ostrinia nubilalis), nondo ambaye hugharimu sekta ya kilimo ya Marekani zaidi ya dola bilioni 1 kila mwaka kama hasara ya mazao na udhibiti wa wasumbufu[4][5].

Watunza bustani wanaweza kuvutia mbawakimia na kwa hivyo kuhakikisha ugavi wa kutosha wa lava kwa kutumia mimea fulani ya rafiki na kuvumilia magugu yenye manufaa. Mbawakimia huvutiwa hasa na Asteraceae, k.m. kaliopsisi (Coreopsis), kosmosi (Cosmos), alizeti (Helianthus) na mchunga (Sonchus), na Apiaceae kama vile bisari (Anethum) na angelika (Angelica).

Spishi za Afrika ya Mashariki[hariri | hariri chanzo]

  • Anapochrysa voeltzkowi
  • Ankylopteryx modesta
  • Ankylopteryx neavei
  • Ankylopteryx pallida
  • Ankylopteryx pusilla
  • Ankylopteryx venusta
  • Apertochrysa eurydera
  • Apertochrysa umbrosa
  • Apochrysa leptalea
  • Apochrysa wagneri
  • Borniochrysa squamosa
  • Brinckochrysa chlorosoma
  • Brinckochrysa lauta
  • Brinckochrysa notabilis
  • Brinckochrysa pulchella
  • Brinckochrysa stenoptera
  • Brinckochrysa tjederi
  • Brinckochrysa turkanensis
  • Ceratochrysa antica
  • Ceratochrysa ceratina
  • Chrysaloysia somalica
  • Chrysemosa commixta
  • Chrysemosa jeanneli
  • Chrysemosa mosconica
  • Chrysemosa senegalensis
  • Chrysocerca nigrivultuosa
  • Chrysoperla comans
  • Chrysoperla congrua
  • Chrysoperla nyerina
  • Chrysoperla plicata
  • Chrysoperla pudica
  • Chrysoperla volcanicola
  • Crassochrysa aculeata
  • Crassochrysa proxima
  • Crassochrysa somalica
  • Cunctochrysa kannemeyeri
  • Dichochrysa atrosparsa
  • Dichochrysa basuto
  • Dichochrysa caffer
  • Dichochrysa chloris
  • Dichochrysa gunvorae
  • Dichochrysa hamata
  • Dichochrysa handschini
  • Dichochrysa incrassata
  • Dichochrysa ingae
  • Dichochrysa kibonotoensis
  • Dichochrysa luaboensis
  • Dichochrysa nicolaina
  • Dichochrysa nyassalandica
  • Dichochrysa perpallida
  • Dichochrysa pervenosa
  • Dichochrysa pulchrina
  • Dichochrysa sansibarica
  • Dichochrysa sjoestedti
  • Dichochrysa spissinervis
  • Dichochrysa varians
  • Dichochrysa venosella
  • Dichochrysa umbrosa
  • Dichochrysa zulu
  • Dysochrysa furcata
  • Glenochrysa principissa
  • Italochrysa asirensis
  • Italochrysa exilis
  • Italochrysa falcata
  • Italochrysa fulvicornis
  • Italochrysa gigantea
  • Italochrysa impar
  • Italochrysa lyrata
  • Italochrysa mozambica
  • Italochrysa peringueyi
  • Italochrysa rufostigma
  • Italochrysa similis
  • Italochrysa variegata
  • Italochrysa zulu
  • Kimochrysa africana
  • Kimochrysa impar
  • Kimochrysa raphidioides
  • Mallada baronissa
  • Mallada boninensis
  • Mallada desjardinsi
  • Nesochrysa illota
  • Nesochrysa marginicollis
  • Nesochrysa rubeola
  • Nesochrysa ruficeps
  • Nesochrysa virgata
  • Pamochrysa stellata
  • Parankylopteryx maculata
  • Parankylopteryx polysticta
  • Parankylopteryx tenuis
  • Parankylopteryx waterloti

Picha[hariri | hariri chanzo]

  1. Henry, C. S., M.L.M. Wells, and C. M. Simon. 1999. Convergent evolution of courtship songs among cryptic species of the carnea-group of green lacewings (Neuroptera: Chrysopidae: Chrysoperla). Evolution 53: 1165Ð1179.
  2. Engel, M.S. & Grimaldi, D.A. (2007) The neuropterid fauna of Dominican and Mexican amber (Neuropterida: Megaloptera, Neuroptera). American Museum Novitates 3587, 1–58.
  3. "Nature's Freddy Krueger". 20 October 2010.  Check date values in: |date= (help)
  4. "European corn borer - Ostrinia nubilalis (Hubner)". entnemdept.ufl.edu. Iliwekwa mnamo 2017-11-13. 
  5. The European Corn Borer | The European Corn Borer. www.ent.iastate.edu. Iliwekwa mnamo 2017-11-13.