Sekunde

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Viambishi awali
vya vipimo sanifu vya kawaida
Jina Kifupi Zao mtiririko
Peta P 1.000.000.000.000.000
Tera T 1.000.000.000.000
Giga G 1.000.000.000
Mega M 1.000.000
Kilo k 1.000
Hekto h 100
Deka da 10
(Kipimo
asilia)
(--)
1
desi d 0.1
senti c 0.01
mili m 0.001
mikro μ 0.000.001
nano n 0.000.000.001
piko p 0.000.000.000.001
femto f 0.000.000.000.000.001

Sekunde (alama: s; pia: nukta, sekundi, sekondi) ni kipimo cha wakati na kati ya vipimo vya kimsingi wa SI.

Kiasili ilihesabiwa kama sehemu ya 60 ya dakika moja lakini kisayansi inapimwa sasa kulingana na mwendo wa mnurulisho wa atomi za sizi -133.

Sekunde sitini (60) ni dakika moja, na sekunde elfu tatu na mia sita (3,600) ni saa moja.

Kisasili siku iligawiwa kwa masaa, masaa kwa dakika na dakika kwa sekundi. Imeonekana ya kwamba hesabu hii haitoshi kwa matumizi ya kisayansi kwa sababu muda wa siku si sawa kamili kutokana na mwendo wa dunia yetu. Hivyo kipimo kamili cha sekunde ilitafutwa kinachopimika katika fizikia na sasa muda wa vipimo vingine vya wakati inahesabiwa kwenye msingi wa sekunde siyo kinyume. Tokeo mojawapo ni ya kwamba siku hailingani tena kamili na masaa 24.

Kwa vipimo vya kisayansi ni muhimu kutaja sehemu za sekunde na hapa viambishi awali vya vipimo sanifu hutumiwa: milisekunde, nanosekunde, femtosekunde. Viambish awali kwa uwingi wa sekunde si kawaida.


Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sekunde kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.