Nenda kwa yaliyomo

Samia Suluhu Hassan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Samia Hassan Suluhu)
Tukio linaendelea

Makala hii inahusu tukio linaloendelea.
Taarifa zinaweza kubadilika haraka kadri tukio linavyoendelea, na vyanzo vya awali vinaweza visiwe vya kuaminika.

Samia Suluhu Hassan


Aliingia ofisini 
17 Machi 2021
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Makamu wa Rais Philip Mpango
mtangulizi John Magufuli

tarehe ya kuzaliwa 27 Januari 1960 (1960-01-27) (umri 65)
Usultani wa Zanzibar
jina ya kuzaliwa Samia Suluhu Hassan
utaifa Mtanzania
chama Chama Cha Mapinduzi
ndoa Hafidh Ameir
watoto Mwanu Hafidh Ameir,Wanu Hafidh Ameir
mhitimu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe
Chuo Kikuu cha Manchester
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
SNHU
dini Uislamu

Samia Suluhu Hassan (alizaliwa 27 Januari 1960) ni Rais wa 6 wa Tanzania na mwanachama wa chama tawala cha Chama Cha Mapinduzi.[1] Kabla ya kuwa rais kutokana na kifo cha John Magufuli, kilichotokea tarehe 17 Machi 2021, Suluhu alikuwa makamu wa rais kwa sababu ya kuwa mgombea mwenza katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.[2]

Tarehe 5 Novemba 2015 aliapishwa kama makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwa mwanamke wa kwanza kufikia cheo hicho, akarudia baada ya uchaguzi mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2020.

Sasa amekuwa rais wa kwanza mwanamke Tanzania na Afrika Mashariki na pia rais wa pili kutoka Zanzibar, wa kwanza akiwa Ally Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya pili.

Uchaguzi wa Oktoba 2025, uliomhakikishia Samia Suluhu Hassan ushindi wa asilimia 97.66 ya kura kadiri ya Tume ya Uchaguzi,[3] uligubikwa na tuhuma za wizi mkubwa wa kura na ukandamizaji mkali wa upinzani. Ujumbe wa waangalizi wa Umoja wa Afrika (AU) ulitangaza kuwa uchaguzi huo "haukuafiki" viwango vya kikanda na kimataifa, ikitaja kasoro nyingi na kukatwa kwa intaneti.[4]

Mashirika mengi ya haki za binadamu yalishutumu serikali yake kwa kuruhusu matumizi ya risasi za moto dhidi ya raia.[onesha uthibitisho] Chama kikuu cha upinzani, Chadema, kilidai kuwa kimekusanya ushahidi wa vifo vya watu 1,000, kikiyaita matukio hayo kuwa ukiukwaji wa haki za binadamu.[3] Serikali ilikanusha madai hayo, huku Rais Hassan akikiri kutokea kwa vifo, alieleza kuwa idadi iliyotolewa na upinzani "imetiwa chumvi kupita kiasi".[5] Wakati awali alikuwa na taswira chanya kama mleta mageuzi, hii imeshuka na kuwa ile ya dikteta[6].

Tarehe 3 Novemba 2025 aliapishwa kwa awamu ya pili na kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maisha ya awali

Suluhu alizaliwa katika Usultani wa Zanzibar.

Alisoma shule za msingi za Chwaka (Unguja), Ziwani (Pemba) na Mahonda (Unguja) katika miaka ya 1966 hadi 1972.

Aliendelea na masomo ya sekondari shule za Ngambo, Unguja (1973-1975) na Lumumba, Unguja (1976).[7]

Baada ya kumaliza masomo yake ya sekondari mnamo 1977, aliajiriwa na Wizara ya Mipango na Maendeleo kama karani. Alifuata kozi fupi kadhaa. Mnamo 1986, alihitimu kutoka Taasisi ya Usimamizi wa Maendeleo (Chuo Kikuu cha Mzumbe cha leo) na diploma ya hali ya juu katika utawala wa umma. [8]

Baada ya kuhitimu, aliajiriwa kwenye mradi uliofadhiliwa na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (World Food Programme). Kati ya miaka 1992 na 1994, alisoma kwenye Chuo Kikuu cha Manchester, Uingereza na kuhitimu stashahada ya uzamili katika uchumi. [9]

Mnamo mwaka 2015, alipata MSc yake katika Maendeleo ya Uchumi wa Jamii kupitia mpango wa pamoja kati ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo Kikuu cha Kusini mwa New Hampshire. [10]

Kazi ya siasa

Mnamo mwaka 2000 aliamua kujiunga na siasa. Aliteuliwa na CCM kama mbunge wa viti maalumu katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar akateuliwa na rais Amani Karume kuwa waziri wa utalii na bishara. Alikuwa mwanamke pekee kwenye ngazi ya mawaziri akaona alidharauliwa na wenzake wa jinsia ya kiume kwa sababu ya jinsia yake. [11] Alichaguliwa tena mnamo 2005 kwenye viti maalum na aliteuliwa tena kama waziri katika wizara ya kazi, jinsia na watoto. [12]

Mwaka 2010 aligombea kwenye uchaguzi kwa Bunge la Kitaifa, akisimama katika jimbo la Makunduchi na kushinda kwa zaidi ya % 80. [13] Rais Jakaya Kikwete alimteua kuwa Waziri wa Nchi wa Mambo ya Muungano. [14] Mnamo 2014, alichaguliwa kama Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba iliyokuwa na jukumu la kuandaa katiba mpya ya nchi. [15] Mnamo tarehe 30 Aprili 2021 alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa CCM [16] akiwa mwenyekiti wa kwanza mwanamke.

Makamu wa Rais

Mnamo Julai 2015, mteule wa urais wa CCM, John Magufuli alimchagua kuwa mgombea mwenza wa uchaguzi wa 2015 na kumfanya kuwa mgombea mwenza wa kwanza mwanamke katika historia ya chama hicho. [17] Baadaye alikuwa makamu wa rais wa kwanza mwanamke katika historia ya nchi kutokana na ushindi wa Magufuli katika uchaguzi. [18]

Maisha ya binafsi

Mnamo 1978 aliolewa na Hafidh Ameir aliye kwa sasa afisa kilimo mstaafu. Wana watoto wanne: binti mmoja na wavulana watatu. [19] Binti yake Wanu Hafidh Ameir (aliyezaliwa 9 Februari 1982), mtoto wa pili, ni mbunge wa viti maalum katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar. [20]

Tanbihi

  1. "Member of Parliament CV". Bunge la Tazania. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-07-13. Iliwekwa mnamo 19 Februari 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Mgombea mwenza Urais 2015 wa Mhe. John Pombe Magufuli ni..
  3. 1 2 (Kiingereza) Tanzania: Killings, Crackdown Follow Disputed Elections, Human Rights Watch, 4 Novemba 2025 (ilifikiwa 6 Novemba 2025)
  4. (Kiingereza) African Union observers slam Tanzania's violent election, African Business, 6 Novemba 2025 (ilifikiwa 6 Novemba 2025)
  5. (Kiingereza) Tanzanian police warn against sharing images following deadly election protests, CNBC Africa (citant Reuters), 5 Novemba 2025 (ilifikiwa 6 Novemba 2025)
  6. "Samia Suluhu Hassan: Tanzania's disputed president – DW – 11/03/2025". dw.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-11-09.
  7. [https://www.bbc.com/swahili/habari/2015/07/150712_profile_ccm_amina_salum_ali Wasifu wa makamu wa rais wa Tanzania Samia Hassan], tovuti ya BBC 13.07 / 05.11. 2015
  8. "Member of Parliament CV". Parliament of Tanzania. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 13 Julai 2015. Iliwekwa mnamo 19 Februari 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  9. https://www.tanzania.go.tz/profiles/profiles/details/138 Ilihifadhiwa 22 Septemba 2020 kwenye Wayback Machine. Profile Details : Former VP of Tanzania, Tovuti ya serikali ya Tanzania, iliangaliwa Machi 2021
  10. "Member of Parliament CV". Parliament of Tanzania. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 13 Julai 2015. Iliwekwa mnamo 19 Februari 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  11. Samia Suluhu Hassan, a tough journey, gazeti la Daily News, tarehe 18 Septemba 2014
  12. Tovuti ya Bunge 2010-2015
  13. Samia Suluhu Hassan, a tough journey, gazeti la Daily News, tarehe 18 Septemba 2014
  14. "Tanzania: History Made as Samia Picked Running Mate". AllAfrica. 13 Julai 2015.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  15. "Tanzania: Union 'Stalwart' Samia Is CA Vice-Chairperson". AllAfrica. 14 Machi 2014.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  16. https://www.bbc.com/swahili/live/habari-56939323
  17. Mohammed, Omar (12 Julai 2015). "Tanzania's ruling party nominates John Magufuli as presidential candidate". Quartz. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 11 Agosti 2015. Iliwekwa mnamo 12 Agosti 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  18. "CCM's John Magufuli declared Tanzania fifth president". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-10-31. Iliwekwa mnamo 2021-03-18.
  19. Samia Suluhu Hassan, a tough journey, gazeti la Daily News, tarehe 18 Septemba 2014
  20. "Hon. Wanu Hafidh Ameir". www.zanzibarassembly.go.tz. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-03-18. Iliwekwa mnamo 2021-03-18.
Alitanguliwa na
John Magufuli
Rais wa Tanzania
2021-
Akafuatiwa na
[[]]
Makala hii kuhusu kuhusu mwanasiasa wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Samia Suluhu Hassan kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.