Mto Morogoro

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mto Morogoro unapatikana katika Mkoa wa Morogoro na ndio ulioupa mji ulio makao makuu ya mkoa (pamoja na mkoa mzima) jina lake.

Inasemekana jina hilo limetokana na sauti ya maji yake katika kutiririka. Lakini wengine wanasema linatokana na upotoshaji wa jina la mwenyeji wa eneo lake, Muruguru (Mluguru).

Maji ya mto huo, unaopitia katikati ya mji wa Morogoro, yanaishia Bahari Hindi kupitia mto Ngerengere na mto Ruvu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]