Masedonia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Eneo la Masedonia la kihistoria limegawanyika leo hii kati ya nchi za kisasa za Ugiriki, Jamhuri ya Masedonia, Bulgaria, Albania na Serbia.
Ramani ya topografia ya Masedonia.

Masedonia (pia: Makedonia) ni eneo la kijiografia na kihistoria kwenye rasi ya Balkani katika Ulaya kusini mashariki.

Katika mwendo wa historia mipaka yake ilibadilika mara nyingi na leo hii ni takriban kilomita za mraba 67,000 zinazohesabiwa humo zinazokaliwa na watu milioni 4,7.

Eneo hili limegawanyika hasa kati ya nchi za Ugiriki, Jamhuri ya Masedonia Kaskazini na Bulgaria; maeneo madogo yamo ndani ya Serbia, Kosovo na Albania.

Katika karne ya 4 KK eneo hili lilikuwa kiini cha ufalme wa Masedonia unaojulikana hasa kutokana na wafalme wake Filipo II na Aleksanda Mkuu. Wakati ule Masedonia ilihesabiwa kama sehemu ya utamaduni wa Ugiriki wa kale.

Baadaye makabila ya Waslavi yalihamia hapa. Leo hii wakazi wengi wa Masedonia ya kihistoria nje ya Ugiriki wanatumia lugha za Kislavoni wakati ndani ya Masedonia ya Kigiriki wanatumia lugha ya Kigiriki.