Mileto

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Maghofu ya thieta ya Mileto.

Mileto (kwa Kigiriki Μῑ́λητος, Mīlētos) kuanzia mwaka 1000 KK hivi ulikuwa mji wa Wayunani huko Karia kwenye mto Meandro unapoishia katika Bahari ya Kati, kwenye pwani ya Uturuki wa leo, karibu na kijiji cha Balat.

Kabla ya uvamizi wa Wapersia katikati ya karne ya 6 KK ulitajwa kuwa mkubwa na tajiri kuliko miji yote ya Wagiriki.

Maghofu yake ni kati ya mahali muhimu pa akiolojia[1][2][3][4][5][6].

Mtume Paulo alifika huko mwaka 58 akakutana na viongozi wa Kanisa la mji jirani, Efeso (Mdo 20:15–38), ambapo alikaa miaka mitatu na kutoka huko alieneza Ukristo katika mkoa mzima wa Asia (Mdo 19:10, 20; 1Kor 16:9).

Inawezekana alirudi tena huko miaka 65-66 kwa kuwa aliandika kwamba aliacha huko Trofimo (2Tim 4:20), na si katika safari ile ya kwanza (Mdo 21:29).

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Olivier Rayet and Thomas, Milet Et Le Golfe Latmique, Fouilles Et Explorations Archeologiques Publ, 1877 (reprint Nabu Press 2010 ISBN 1-141-62992-5
  2. Theodor Wiegand and Julius Hülsen [Das Nymphaeum von Milet, Museen zu Berlin 1919] and Kurt Krausem, Die Milesische Landschaft, Milet II, vol. 2, Schoetz, 1929
  3. Theodor Wiegand et al., Der Latmos, Milet III, vol. 1, G. Reimer, 1913
  4. Carl Weickert, Grabungen in Milet 1938, Bericht über den VI internationalen Kongress für Archäologie, pp. 325-332, 1940
  5. Carl Weickert, Die Ausgrabung beim Athena-Tempel in Milet 1955, Istanbuler Mitteilungen, Deutsche Archaeologische Institut, vol. 7, pp.102-132, 1957
  6. Carl Weickert, Neue Ausgrabungen in Milet, Neue deutsche Ausgrabungen im Mittelmeergebiet und im Vorderen Orient, pp. 181-96, 1959

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Gorman, Vanessa B. (2001). Miletos, the Ornament of Ionia: A History of the City to 400 BCE. Ann Arbor, MI: Michigan University Press. ISBN 9780472111992. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Uturuki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mileto kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.