Samotrake

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kijiji cha Samotrake, na Mlima Fengari nyuma yake.

Samotrake (kwa Kigiriki: Σαμοθράκη, samoˈθraci) ni kisiwa cha Ugiriki kilichoko kaskazini mwa Bahari ya Aegean.

Kina wakazi 2,859 (2011) wanaotegemea zaidi uvuvi na utalii.

Kinatajwa na Biblia ya Kikristo kwa kuwa mwaka 49 au 50 Mtume Paulo, katika safari yake ya pili ya kimisionari, aliabiri kutoka Troas hadi Samotrake akielekea Makedonia kutokana na njozi aliyoipata ikiwa na himizo la kuingia Ulaya ili kuwaletea Injili Wamakedonia.

Matendo ya Mitume 16:11 kinasimulia hivi: "Basi tukang’oa nanga kutoka Troa, tukafika Samothrake kwa tanga moja, na siku ya pili tukafika Neapoli".

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Michel Mourre, Dictionnaire Encyclopédique d'Histoire, article "Samothrace", Bordas, 1996
  • Marcel Dunan, Histoire Universelle, Larousse, 1960

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Ugiriki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Samotrake kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.