Washington, D.C.

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mji wa Washington, D.C.






Jiji la Washington

Bendera
Jiji la Washington is located in Marekani
Jiji la Washington
Jiji la Washington

Mahali pa mji wa Washington katika Marekani

Majiranukta: 38°54′36″N 77°0′36″W / 38.91000°N 77.01000°W / 38.91000; -77.01000
Nchi Marekani
Tovuti:  http://www.dc.gov/
kwa maana mbalimbali ya jina "Washington" tazama Washington (maana)
Nguzo ya Washington na Nyumba Nyeupe (White House)

Washington D.C. ni mji mkuu wa Marekani mwenye wakazi 553,523. Kifupi "D.C." baada ya jina chamaanisha "District of Colombia" ambayo ni mkoa wa shirikisho yaani eneo lililotengwa moja kwa moja kwa vyombo vya shirikisho la Marekani kwa sababu maeneo mengine ya Marekani yako chini ya majimbo mbalimbali yanayojitawala.

Jina la mji mkuu limechaguliwa kwa heshima ya kiongozi wa uhuru na rais wa kwanza George Washington. Jina la "District of Colombia" likachaguliwa kwa heshima ya Kristoforo Kolumbus mpelelezi wa Amerika.

Mji wa Washington uko kando la mto Potomac kati ya majimbo ya Maryland na Virginia. Uko karibu na pwani la mashariki la Marekani. Hori ya Chesapeake ya Atlantiki iko 35 km kutoka mji. Anwani ya kijiografia ni 38°53'42"N na 77°2'12"W.

Washington D.C. ni tofauti na jimbo la Washington lililopo upande wa magahribi wa Marekani.

Hapa ni makao rasmi ya Bunge la Marekani, ya Rais pamoja na serikali yake na makao ya mahakama kuu. Kuna pia majengo ya kihistoria hata kama Marekani haina historia ndefu pamoja na makumbusho mazuri.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Makao ya kwanza ya serikali ya Marekani ilikuwa New York. Rais George Washington mwenyewe alichagua eneo la mji mpya kando la mto Potomac mwaka 1790. Ujenzi wa ikulu la Nyumba Nyeupe ulianza 1792. Mpango wa mji ulifuata mfano wa mji wa Karlsruhe (Ujerumani).

11. Juni 1800 Washington ikawa mji mkuu wa Marekani. Wakati wa vita ya Uingereza na Marekani ya 1814 mji ulivamiwa na kuchomwa na Waingereza.

Hadi vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Marekani Washington ilikuwa mji mdogo usiozidi wakazi 75,000 lakini ilikua baada ya vita kwa sababu serikali iliongezeka idara na wafanyakazi.

Tangu 1878 mji wa Washington na mkoa wa shirikisho ("D.C.") viliunganishwa. Mji kama mkoa ulitawaliwa moja kwa moja na bunge. Tangu 1973 mji umempata meya na serikali ya kimanisipaa. Kwenye bunge lenyewe hakuna mbunge wa wakazi wa Washington. Kuna mwakilishi wao mle lakini hana kura.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]


Majimbo na maeneo ya Marekani
Majimbo ya Marekani
AlabamaAlaskaArizonaArkansasCaliforniaColoradoConnecticutDelawareFloridaGeorgiaHawaiiIdahoIllinoisIndianaIowaKansasKentuckyLouisianaMaineMarylandMassachusettsMichiganMinnesotaMississippiMissouriMontanaNebraskaNevadaNew HampshireNew JerseyNew MexicoNew YorkNorth CarolinaNorth DakotaOhioOklahomaOregonPennsylvaniaRhode IslandSouth CarolinaSouth DakotaTennesseeTexasUtahVermontVirginiaWashingtonWest VirginiaWisconsinWyoming
Mkoa wa Mji Mkuu
Mkoa wa Columbia (Washington D.C.)
Visiwa vya ng'ambo
Katika Pasifiki: Samoa ya MarekaniVisiwa vya Mariana ya KaskaziniGuamKatika Karibi: Puerto RicoVisiwa vya Virgin vya MarekaniVisiwa vidogo sana vya Pasifiki:Kisiwa cha HowlandKisiwa cha Jarvis Atolli ya JohnstonKingman ReefAtolli ya MidwayKisiwa cha BakerAtolli ya PalmyraKisiwa cha WakeKisiwa kidogo cha Karibi: Kisiwa cha Navassa
Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Washington, D.C. kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons