St. Pierre na Miquelon
| |||
Wito: A mare labor (Kazi kutoka bahari) | |||
Lugha rasmi | Kifaransa | ||
Mji Mkuu | St. Pierre | ||
Rais wa Halmashauri Kuu | Stéphane Artano | ||
Mkuu wa Mkoa (Préfet) | Albert Dupuy | ||
Eeno – Jumla – % maji |
242 km² 0.0% | ||
Idadi ya wakazi – Jumla (2011) |
6,080 | ||
Pesa | Euro (€;EUR) | ||
Jamla la pato la eneo (Wanazaa kiasi gani cha mali kwa mwaka) |
$48.3 Millioni | ||
Kanda la saa | UTC-3 | ||
Simu ya eneo | 508 ¹ | ||
Intaneti TLD | .pm | ||
1. 0508 kutoka Ufaransa bara. | |||
![]() |
Saint-Pierre na Miquelon ni funguvisiwa na eneo la ng'ambo la Ufaransa (kwa Kifaransa "Collectivité d'outre mer") karibu na pwani ya Kanada katika bahari ya Atlantiki.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Funguvisiwa iko karibu na jimbo la Newfoundland ya Kanada.
Visiwa vikubwa zaidi ni Saint-Pierre (km² 26), Miquelon (km² 110), Langlade (km² 91) halafu kuna visiwa vingine vidogo. Jumla la eneo ni km² 242 lenye wakazi 6,080, hasa kisiwani Saint-Pierre (5,456).
Karibu wote wanaongea Kifaransa na ni waamini wa Kanisa Katoliki.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Visiwa vimetembelewa na wavuvi kutoka Ulaya tangu karne ya 15.
Inaaminiwa ya kwamba makazi ya kwanza ya kudumu ya wavuvi Wafaransa yalianzishwa katika karne ya 17.
Tangu vita ya miaka saba visiwa hivi vilikuwa mabaki pekee ya koloni la Kanada ya Kifaransa.
Uchumi[hariri | hariri chanzo]
Uchumi umetegemea tangu mwanzo uvuvi. Siku hizi kuna pia utalii.
Siasa[hariri | hariri chanzo]
Wakazi wa visiwa ni raia wa Ufaransa. Huchagua bunge lao lenye watu 19. Bunge la eneo linamchagua mwakilishi mmoja katika bunge la kitaifa la Ufaransa.
Saint-Pierre na Miquelon si sehemu ya Eneo la forodha la Ulaya.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Official tourism website for St Pierre and Miquelon
- Tourism ressources and information
- Le Phare: Association of Tourism Professionals
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|