Isopodi mkubwa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Isopodi mkubwa
Isopodi mkubwa
Isopodi mkubwa
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Faila: Arthropoda
Faila ya chini: Crustacea
Oda: Isopoda
Oda ya chini: Cymothoida
Familia: Cirolanidae
Jenasi: Bathynomus
Ngazi za chini

Spishi 20:

Isopodi wakubwa ni miongoni ya takriban spishi 20 za isopodi (gegereka wanaohusiana kwa mbali na kamba na kaa, ambao ni dekapodi) katika jenasi Bathynomus. Wapo tele katika maji baridi na ya kina ya bahari za Atlantiki, Pasifiki na Hindi[1][2]. Hakuna spishi karibu na pwani ya Afrika ya Mashariki.

Bathynomus giganteus mara nyingi huchukuliwa kama isopodi mkubwa kabisa duniani, lakini inawezekana kuna spishi nyingine kubwa vile, ambazo hazikufanyiwa utafiti bado, zinaweza kufika ukubwa sawa (kwa mfano, Bathynomus kensleyi)[1].

Mtafiti wa zoolojia Mfaransa Alphonse Milne-Edwards alikuwa wa kwanza [3] kuelezea jenasi hiyo katika mwaka wa 1879 [4] baada ya mwenzake Alexander Agassiz kumpata Bathynomus giganteus kijana wa kiume kutoka Ghuba ya Meksiko; huu ulikuwa ni ugunduzi wa kusisimua kwa wanasayansi na umma kwa sababu wakati ule wataalamu walikuwa bado wakivutana juu ya swali kama uhai unawezekana katika vilindi vikubwa vya bahari. Bathynomus giganteus wa kike hawakupatikana hadi mwaka 1891.

Isopodi wakubwa hawawavuti sana wavuvi wa kibiashara zaidi, kutokana na uhaba wa upatikanaji wake. Sampuli chache zilizokamatwa katika Amerika na Japani kwa mitego ya chambo wanaweza kutazamwa mahali pachache huko Marekani na Japani katika tangisamaki za umma.

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

Muonekano wa mbele wa Bathynomus giganteus, kuonyesha macho yake makubwa

Isopodi mkubwa ni mfano mzuri wa viumbe vikubwa kabisa katika kina cha bahari, vile ni wakubwa zaidi ya isopodi wa kawaida ambao ni hadi sentimita 5 (inchi 2.0).

Bathynomus anaweza kugawanywa katika spishi ya "wakubwa" ambapo waliokua kwa ujumla ni kati ya sentimita 8 na 15 (inchi 3.1 na 5.9) kwa urefu na spishi ya "wakubwasana" ambapo waliokua kwa ujumla ni kati ya sentimita 17 na 50 (inchi 6.7 na 19.7). [1] Mmoja ya wale "mkubwasana", Bathynomus giganteus, anafikia urefu wastani kati ya sentimita 19 na 36 (inchi 7.5 na 14.2), [3] akiwa na uzito na urefu wa takriban kilo 1.7 na sentimita 76 (inchi 30) kwa mtiririko huo. [5]

Mofolojia yao inafanana na ya binamu zao terestria, ambao ni woodlouse: kama baadhi ya woodlice, pia wana uwezo wa kujikunja kama "mpira", ambapo gamba gumu tu linabaki wazi. Hii hutoa ulinzi dhidi ya wahasimu wanapojaribu kuwashambulia upande wa chini ambao ni dhaifu zaidi. Sehemu ya kwanza ya gamba imeungwa na kichwa; vipande vya chini zaidi (matakoni) navyo pia vimeungwa, kutengeneza "ngao ya caudal" juu ya fumbatio fupi (pleon). [3] Macho yao makubwa ni mchanganyo wa karibia vipengere, na sessile 4,000, na yapo mbali mbali juu ya kichwa.

Kuna jozi mbili za antena. Miguu ya uniramous thoracic au pereiopods imepangiliwa katika jozi saba, ya kwanza ambayo imerekebishwa katika maxillipeds hushika na kuleta chakula kwenye seti nne za taya. Fumbatio lina sehemu tano zinazoitwa pleonites, kila moja ikiwa na jozi ya biramous pleopods; hizi zimebadilishwa kuwa miguu ya kuogelea na rami, maumbile bapa ya kupumulia yafanyayo kazi kama gills. Isopodi ni lilaki hafifu au waridi kwa rangi. [1][2]

Safu[hariri | hariri chanzo]

Isopodi wakubwa wamerekodiwa katika Atlantiki ya Magharibi kutoka Georgia (USA) hadi Brazili, ikiwa ni pamoja na Ghuba ya Meksiko na Karibi. [1] Spishi tatu zijulikanazo za Atlantiki ni Bathynomus obtusus, Bathynomus miyarei na Bathynomus giganteus, na wa mwisho wa hawa alirekodiwa kutoka Marekani tu. [1] Spishi nyingine zote zilizobakia zimezuiwa katika Indo-Pasifiki. [1] Isopodi mkubwa hajulikani kutoka Atlantiki Mashariki au Pasifiki ya Mashariki. [1] Spishi kubwa kabisa (spishi tano) ni utajiri upatikanao Mashariki mwa Australia.

Ikolojia[hariri | hariri chanzo]

Upande wa chini wa Bathynomus giganteus

Isopodi mkubwa ni mwokotezaji muhimu katika mazingira ya kina kirefu cha bahari ya benthic; hasa wakipatikana kutoka ukanda wa utusiutusi wa sublittoral katika urefu wa mita 170 (futi 560) hadi eneo la giza zito bathypelagic katika mita 2,140 (futi 7,020), ambapo shinikizo ni kubwa na joto liko chini sana. [6]

Spishi chache tu kutoka jenasi hii zimeripotiwa kutoka kina kifupi, hasa Bathynomus miyarei kati ya mita 22 na mita 280 (futi 72 na 919), [7] asiyejulikana vizuri Bathynomus decemspinosus kati ya mita 70 na 80 (futi 230 na 260) na Bathynomus doederleini katika kina kifupi kama mita 100 (futi 330). [1]

Kumbukumbu za kina cha maji kwa isopodi mkubwa yeyote ni mita 2,500 (futi 8,200) kwa Bathynomus kensleyi, lakini spishi hii pia hutokea katika kina kifupi kama mita 300 (futi 980). [1] Zaidi ya asilimia 80 ya Bathynomus giganteus wanapatikana katika kina cha kati ya mita 365 na 730 (futi 1,198 na 2,395). [8] Katika maeneo yenye spishi ya "wakubwa" na "wakubwasana", wa awali hasa huishi kwenye mteremko wa bara, wakati huyu wa mwisho huishi hasa kwenye ubapa wa bathyal. [1]

Ingawa Bathynomus warekodiwa kukutwa katika maji vuguvugu kama 20 °C (68 °F), wao hupatikana hasa katika maeneo ya baridi sana. [9] Kwa mfano, wakati wa utafiti wa fauna wa kina kirefu cha bahari ya Exuma sound nchini Libya, Bathynomus giganteus alipatikana kwamba wa kawaida katika maji kati ya 3.25 na 13 °C (37.8 na 55.4 °F), lakini wengi zaidi katika joto la chini. [10] Kwa kulinganisha, matokeo ya awali yanaonyesha kwamba Bathynomus doederleinii huacha ulishaji wakati hali ya joto iko chini ya 3 °C (37 °F). [11] Ukomo huu wa hali joto ya chini unaweza kuelezea ukosekanifu wao katika maeneo ya ukanda wa baridi ambapo bahari katika vina vinavyopendwa zaidi na Bathynomus mara nyingi ni baridi. [11] Wao wanadhaniwa kupendelea tabaka la chini lenye tope au udongo mfinyanzi linalopelekea maisha ya faragha.

Ingawa kwa kawaida ni waokotezaji, isopodi hawa hasa ni wala nyama na hula nyangumi wafu, samaki na ngisi; pia wanaweza kuwinda wanyama wanaosonga polepole kama vile sea cucumbers, sponges, radiolarians, wadudu, na zoobenthos wengineo, na pengine hata samaki hai. Wao wanajulikana kwa kushambulia samaki waliokamatwa na mvulio.

Isopodi mkubwa mmoja alipigwa pichamwendo akimshambulia papa dogfish mkubwa katika mtego wa maji ya kina kirefu kwa kujikia na kula uso wa mnyama. [12] Kama chakula ni haba katika biome ya kina kirefu cha bahari, isopodi mkubwa huishi kwa kukabiliana na chochote kinachokuja mbele yake; wamezoea vipindi virefu vya njaa na wamejulikana kuishi miaka mitano bila chakula wakiwa mateka. [13][14]

Wakati wanakutana na chanzo muhimu cha chakula, isopodi wakubwa wanakula kwa ulafi kufikia kiwango cha kuhatarisha uwezo wao wa kujongea. Mtaala kuchunguza yaliyomo katika mfumo wa umeng'enyaji wa mwaka 1651 sampuli za Bathynomus giganteus zilionyesha kwamba kumbe samaki waliliwa zaidi, ikifuatiwa na cephalopods na decapods, hasa carideans na galatheids. [3]

Isopodi wakubwa waliokusanywa katika mwambao wa Mashariki ya Australia kwa kuweka mitego wameonyesha mbadala katika utofauti na kina cha maji. Vile kina cha maji kinavyozidi kuwa kikubwa, idadi chache ya spishi kupatikana, na spishi walio wakubwa waelekeao kuwepo. Isopodi wakubwa waliopatikana katika maji ya kina kirefu sana huko Australia walifananishwa na wale walioonekana Meksiko na India.

Kulingana na kumbukumbu ya kisukuku inafikiriwa kwamba Bathynomus walikuwepo zaidi ya miaka milioni 160 iliyopita, kabla ya mvunjiko wa barakuu Pangaia, hivyo hawakubadilika kwa kujitegemea katika maeneo yote matatu, lakini tangia hapo inaweza kutarajiwa kwamba Bathynomus wanaonyesha mageuko tofauti katika maeneo mbalimbali. Hata hivyo isopodi wakubwa katika maeneo yote matatu walikuwa karibu kufanana katika muonekano [15] (Ingawa kuna tofauti kadhaa, na ni spishi tofauti). [1] Huu mpunguo wa muachano wa phenotypic unaunganishwa kwenye ngazi za mwanga wa chini sana wa makazi yao. [15]

Uzazi[hariri | hariri chanzo]

Utafiti wa msimu wa uwingi wa Bathynomus giganteus vifaranga na waliokua unapendekeza kilele katika uwezo wa uzazi katika miezi ya majira ya kuchipua na majira ya baridi. Hii inaonekana kuwa hivi kutokana na uhaba wa chakula wakati wa majira ya joto.

Wale wa kike wazima hukuza mfuko wa makinda au marsupium wakati wapo tayari kwa tendo. Isopodi wadogo huibuka kutoka marsupium kama mfano mdogo wa waliokua, wajulikanao kama mancae. Hii si awamu ya kiluwiluwi: mancae ni wamekua kikamilifu, wamekosa tu jozi ya mwisho ya pereiopod.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.00 1.01 1.02 1.03 1.04 1.05 1.06 1.07 1.08 1.09 1.10 1.11 1.12 Lowry, J. K. and Dempsey, K. (2006). The giant deep-sea scavenger genus Bathynomus (Crustacea, Isopoda, Cirolanidae) in the Indo-West Pacific. In: Richer de Forges, B. and Justone, J.-L. (eds.), Résultats des Compagnes Musortom, vol. 24. Mémoires du Muséum National d’Histoire Naturalle, Tome 193: 163–192.
  2. 2.0 2.1 Mike Krumboltz. "Sea Creature Surfaces, Chaos Ensues", Yahoo! Canada News, April 1, 2010. Retrieved on 2016-11-06. Archived from the original on 2010-04-09. 
  3. 3.0 3.1 3.2 3.3 Briones-Fourzán, Patricia; Lozano-Alvarez, Enrique (1991). "Aspects of the biology of the giant isopod Bathynomus giganteus A. Milne Edwards, 1879 (Flabellifera: Cirolanidae), off the Yucatan Peninsula". Journal of Crustacean Biology 11 (3): 375–385. JSTOR 1548464. doi:10.2307/1548464. 
  4. Milne-Edwards, A. (1879). "Sur un isopode gigantesque des grandes profondeurs de la mer" [On a giant isopod from the deep ocean]. Comptes rendus de l'Académie des Sciences (in French) 88: 21–23. 
  5. "Monster of the deep: Shocked oil workers catch TWO-AND-A-HALF-FOOT 'woodlouse'", April 3, 2010. 
  6. Kigezo:Cite thesis
  7. Bathynomus miyarei. SeaLifeBase (23 March 2010). Iliwekwa mnamo 26 February 2012.
  8. Holthuis, L. B.; Mikulka, W. R. (1972). "Notes on the deep-sea isopods of the genus Bathynomus A. Milne-Edwards, 1879". Bulletin of Marine Science 22: 575–591. 
  9. Bathynomus giganteus' gigantisme. University of Amsterdam (10 February 2014). Iliwekwa mnamo 14 January 2016.
  10. The assessment of deep sea distribution and abundance of scavenging fauna in the Exuma Sound. Fisheries Conservation Foundation (10 February 2014). Iliwekwa mnamo 14 January 2016.
  11. 11.0 11.1 Wetzer, R. (1986). "Bathynomus, A living Sea monster". Terra 25 (2): 26–29. 
  12. "Alien Sharks: Close Encounters". Shark Week (Discovery Channel). 6 July 2015.
  13. Gallagher, Jack (2013-02-26). Aquarium's deep-sea isopod hasn't eaten for over four years. The Japan Times. Iliwekwa mnamo 2013-05-21.
  14. I Won't Eat, You Can't Make Me! (And They Couldn't). NPR (February 22, 2014). Iliwekwa mnamo February 23, 2014.
  15. 15.0 15.1 Parker, A. (2003). In the Blink of an Eye: How Vision Kick-started the Big Bang of Evolution. The Free Press. pp. 121–132. ISBN 0-7432-5733-2. 
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Isopodi mkubwa kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.