Mtumiaji:Zenman/Mradi wa Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Makala iliyochaguliwa[hariri | hariri chanzo]

Makala iliyochaguliwa kwa Aprili 2012[hariri | hariri chanzo]

Faili:Askari.jpeg
Askari wa jeshi la kijerumani

Kampeni za Afrika ya Mashariki ulikuwa mfululizo wa mapigano ya kivita yaliyotokea Afrika ya Mashariki ya Kijerumani (Tanganyika, Rwanda na Burundi ya leo) na koloni jirani za Msumbiji, Rhodesia ya Kaskazini (Zambia), Afrika ya Mashariki ya Kiingereza (Kenya), Uganda, na Kongo ya Kibelgiji. Kampeni hizi zilianza mwezi wa Agosti 1914 zikaisha rasmi mnamo mwezi wa Novemba katika mwaka wa 1918. Wapiganaji katika vita hii walikuwa jeshi la kikoloni cha Kijerumani lililofanywa hasa na askari Waafrika waliosimamiwa na maafisa Wajerumani pamoja na walowezi Wajerumani na wanamaji wa manowari waliokaa Afrika ya Mashariki wakati wa mwanzo wa vita 1914. Dhidi yao walisimama jeshi dogo la kikoloni la Kiingereza katika Kenya na Rhodesia, halafu vikosi vya jeshi la kikoloni la Uhindi ya Kiingereza na vikosi kutoka Afrika Kusini.


Je, wajua...?[hariri | hariri chanzo]


Wasifu Uliochaguliwa[hariri | hariri chanzo]

Wasifu Uliochaguliwa kwa Aprili 2012[hariri | hariri chanzo]

Robert Mugabe (2009)

Robert Gabriel Mugabe (* 21 Februari 1924) amekuwa kiongozi wa Zimbabwe tangu 1980. Yeye ni mwenyekiti wa chama tawala cha ZANU. 1980 alikuwa waziri mkuu na 1987 Rais wa Zimbabwe. Kabla ya wakati ule aliongoza upinzani wa ZANU dhidi ya serikali ya walowezi Waingereza nchini waliofuata siasa ya ubaguzi wa rangi. Mugabe alirudiwa katika uchaguzi mbalimbali. Tangu mwaka 2000 uchaguzi hizi zimekuwa mashakani kutokana na matishio na matumizi ya mabavu dhidi ya wapinzani. Utawala wa Mugabe umeitwa wa kidikteta tangu mwaka 2002. Kutokana na mashataka dhidi ya serikali ya Mugabe ya kudharau haki za binadamu nchi Zimbabwe ilisimamishwa ndani ya Jumuiya ya Madola.


kuchaguliwa picha kwa 2012[hariri | hariri chanzo]

kuchaguliwa picha kwa Aprili 2012[hariri | hariri chanzo]


Apalis flavida kutoka Abuko, Gambia.
(kupata bango)