Ushirikina

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Udongo hamsa kwenye ukuta; uliaminiwa kulinda wenyeji wa nyumba kutoka madhara.

Ushirikina ni wazo ambalo halina sababu yenye msingi katika maarifa au mang'amuzi. Neno hili hutumiwa kwa kutaja imani ambazo hazina msingi. Hii inasababisha baadhi ya ushirikina kuitwa "Hadithi za kale za wake". Pia kwa kawaida hutumiwa katika imani na mazoea zinazohusu bahati au utabiri ambapo matukio ya baadaye yanabashiriwa na matukio yasiyohusiana.

Ushirikina kadiri ya Uislamu[hariri | hariri chanzo]

Neno hiko limetoka kwenye lugha ya Kiarabu, "shirk" ikiwa na maana ya kumfanya Mwenyezi Mungu kuwa na mtu wa kumsaidia au kumpa asiyekuwa mungu nguvu za kiungu ikiwa ni pamoja na kumuabudu, kumnyenyekea na kumuogopa.

Watu wengi wamekuwa wakilitumia vibaya neno ushirikina. Wanahusisha neno hilo na uchawi. Ushirikina na uchawi ni vitu viwili tofauti na ushahidi wa hili hutokana na mafundisho ya imani ya Kiislamu. Mtume Muhammad ambaye ni mtume wa mwisho kwa mujibu wa Uislamu amefundisha kuwa miongoni mwa madhambi saba yenye kumuangamiza mtu mbele ya Mungu wake ni ushirikina, uchawi na mengine matano. Kwa mujibu wa maneno hayo ya mtume Muhammad tunaona fika kuwa ushirikina na uchawi ni vitu viwili tofauti. Hivyo kwa Uislamu ushirikina ni kuabudu asiyekuwa Mungu. Inawezekana mtu akaabudia jiwe, kuku, ng'ombe, jini, jua na kitu au kiumbe kingine chochote kwa kukitii na kukinyenyekea.

Ushirikina kadiri ya Kilatini[hariri | hariri chanzo]

Katika Kilatini neno ni superstitio na linamaanisha "kusimama juu", hivyo: "mshangao wa ajabu, hasa wa Kimungu" au "kusadiki mno".

Neno hili lilitumika katika karne ya 1 KK, hasa katika maandishi ya Cicero, Livy, Ovid, likimaanisha imani ambazo zimezidisha au hazina msingi kwa hofu au uchawi hasa wa kigeni.

Ushirikina na hadithi[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na wasomi kutoka Ulaya neno lilitumiwa na imani yoyote iliyopinga Ukristo; leo linatumika kama dhana bila ya msingi katika sayansi, mantiki na maarifa.

Ushirikina mwingi Ulaya unasemekana ulitokana na magonjwa yaliyofagia Ulaya.

Ushirikina na dini[hariri | hariri chanzo]

Kulingana na asili ya neno la Kilatini, waumini wa dini fulani mara nyingi huchukulia dini nyingine kama ushirikina. Vilevile wakanamungu wanaweza kuona imani ya dini yoyote kama ushirikina.

Vitendo vingine vya kidini huchukuliwa na watu wa nje kama "ushirikina" wakiona tukio fulani kuwa la ajabu (miujiza, maisha baada ya kufa, utendaji wa Kimungu au kuloga).

Wagiriki na Warumi ambao walitengeneza uhusiano wao na miungu kwa msingi wa masharti ya kisiasa na ya kijamii, walikemea mtu ambaye daima alitetemeka na hofu mbele ya miungu, kama vile mtumwa alivyoogopa bwana mkatili. "Hofu hiyo ya miungu ulijulikana na Warumi kama ushirikina [1].

Pengine asili ya ushirikina ni desturi za kidini ambazo ziliendelea kuzingatiwa na watu ambao hawazingatii tena dini iliyozaa mazoeza hayo. Mara nyingi desturi hizo zilipotewa na maana katika mchakato huu.

Katika kesi nyingine, ilichukuliwa na mazoea ya sasa ya dini ya muumini. Kwa mfano, wakati wa kugeuza watu kuwa Wakristo Ulaya, alama za awali za wasiomuamini Mungu zilibadilishwa na matumizi ya msalaba.

Kanisa Katoliki linachukulia ushirikina kama dhambi kwa kuwa unaashiria utovu wa uaminifu katika vitendo vya Mungu na vile vile ni ukiukaji wa amri ya kwanza kati ya Amri Kumi.

Katekisimu ya Kanisa Katoliki inaashiria kuwa ushirikina "unawakilisha hisia mbaya za dini" (para. # 2110).

Mafundisho hayo yanakanusha madai kuwa mafundisho mengine ya Kikatoliki ni ya ushirikina:

Ushirikina ni kwa hisia ya kidini na mazoea ya hisia hii. Inaweza hata kuathiri ibada ya kweli tunayomtolea Mungu, kwa mfano, wakati mtu anachukulia umuhimu katika kuwa miujiza kwa vitendo fulani halali au ya lazima. Ili kuelekea katika sala au ishara za sakramenti katika utendaji wa nje, mbali ya mambo ya ndani ambapo wanahitaji ushirikina. (Taz. Math 23:16-22) [2]

Ushirikina na saikolojia[hariri | hariri chanzo]

Mwaka 1948 daktari wa saikolojia na tabia B. F. Skinner alichapisha makala katika jarida la Experimental Psychology, ambapo alielezea njiwa wake walionyesha tabia ya ushirikina. Njiwa mmoja alijivingirisha katika ngome yake, mwingine alitikisa kichwa chake katika mwendo wa pendulum, wakati wengine walionyesha tabia tofauti. Kwa kuwa hizi tabia zilifanywa kwa lengo la kupata chakula kutoka stoo, ingawa ilikuwa imeashiriwa kumwachilia chakula katika muda uliopangwa bila ya kujali vitendo vya namna hiyo, Skinner aliamini kwamba njiwa walikuwa wakijaribu kubadilisha kwa kufanya vitendo hivyo. Yeye alipitisha jambo hilo kama pendekezo kuhusu asili ya tabia ya ushirikina katika binadamu.

Wanasaikolojia wengine kama vile Staddon na Simmelhag walitoa maelezo mbadala.

Licha ya changamoto katika utafsiri wa Skinner wa msingi wa tabia za ushirikina za njiwa wake, kielelezo chake kimetumika kuelezea tabia ya ushirikina katika binadamu.

Mwanzoni, katika utafiti wa Skinner, "baadhi ya njiwa waliitika hadi mara 10,000 bila kulazimishwa, ambapo hapo awali walikuwa na ratiba ya kusisitiza. Ikilinganishwa na ratiba zingine (k.m. uwiano ulio thabiti, muda ulio thabiti), tabia hizo zilikuwa sugu kupotea.

Hii inaitwa athari ya kudhibitisha ambako si kamili, na hii kutumika kuelezea tabia ya ushirikina katika binadamu. Kuwa sahihi zaidi, athari hii inamaanisha kwamba, wakati mtu anapofanya tendo akitarajia kusaidiwa, na hakuna usaidizi wowote, ni kweli kuwa inajenga hisia ya kuwepo ndani ya mtu binafsi.

Hii inatia nguvu tabia ya ushirikina kwa binadamu kwa binadamu kwa sababu mtu anaona kwamba, kwa kuendelea hatua hii, usaidizi utakuja; au kwamba usaidizi ulikuja wakati fulani hapo awali kwa ajili ya hatua hiyo, ingawa si wakati wote, lakini hii inaweza moja ya nyakati hizo.

Kutoka mtazamo ulio rahisi, uteuzi asili utapendelea kushinikiza tabia itakayozalisha uhusiano dhaifu. Iwapo kuna faida sahihi ya kuunda uhusiano thabiti, basi hii itaweza kuondoa mtazamo wa kuogopa kutengeneza uhusiano wa "ushirikina" usiofaa.

Angalia pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. (Veyne 1987, p 211)
  2. (para. # 2111)
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.